Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 21:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Lakini mbele mambo hayo yote yatokee, mutakamatwa na kuteswa. Watawapeleka kwenda kuhukumiwa katika nyumba za kuabudia na kuwatia katika vifungo. Vilevile mutapelekwa mbele ya wafalme na ya wakubwa kwa ajili ya jina langu,

Gade chapit la Kopi




Luka 21:12
31 Referans Kwoze  

Kwa ajili ya utukufu wa Bwana, mutii mamlaka yote ya watu: ikiwa ni mufalme anayekuwa na uwezo juu ya vyote,


Kesho yake, jemadari alitaka kujua mashitaki kamili ya Wayuda juu ya Paulo. Kwa hiyo akamufungua na kuamuru wakubwa wa makuhani pamoja na Baraza Kubwa wafanye mukutano. Kisha akamuleta Paulo na kumusimamisha mbele yao.


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


Lakini Saulo aliendelea kuteketeza kanisa, akiingia nyumba kwa nyumba, na kuwakamata waamini, wanaume na wanawake, na kwenda kuwatupa katika kifungo.


Wajumbe wa baraza wakakubali shauri la Gamalieli. Halafu wakawaita mitume, wakawapiga fimbo na kuamuru wasifundishe tena kwa jina la Yesu. Kisha wakawaacha kwenda.


Mukumbuke maneno niliyowaambia kwamba mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake. Kama walinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile. Na kama walishika maneno yangu, watashika maneno yenu vilevile.


na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatesa na kuwaua.


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Na haya yote ni kama mwanzo wa maumivu ya kuzaa tu.


Kutakuwa tetemeko kubwa la inchi. Vilevile kutakuwa njaa na magonjwa makali kwenye nafasi mbalimbali. Zaidi ya ile kutakuwa mambo ya kuogopesha na vitambulisho vya ajabu toka mbinguni.


Lakini watawafanyia ninyi haya yote kwa ajili yangu, kwa sababu hawamujui yule aliyenituma.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite