Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 20:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Lakini wale walimaji walipomwona akikuja, wakasemezana: ‘Musimame! Huyu ndiye atakayerizi shamba hili. Basi tumwue kusudi shamba hili lipate kuwa urizi wetu.’

Gade chapit la Kopi




Luka 20:14
20 Referans Kwoze  

Na kama sisi ni watoto, basi tutakuwa na sehemu katika urizi ule Mungu aliowaahidi watu wake, na tutashiriki pamoja na Kristo katika urizi ule; kwa maana kama tukiteswa pamoja naye tutatukuzwa pamoja naye vilevile.


Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.


Halafu mukamwua yule anayekuwa asili ya uzima, lakini Mungu amemufufua. Na sisi ni washuhuda wa jambo hilo.


Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.


Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walitafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliogopa watu.


Saa ile ile wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakatafuta kumukamata, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao.


Nao wakaanza kupiga mafikiri pamoja na kusema: “Kama tukijibu kwamba mamlaka yake yalitoka kwa Mungu, atauliza: ‘Kwa sababu gani basi hamukumwaminia?’


Yesu alikuwa akifundisha kila siku ndani ya hekalu. Lakini wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria pamoja na wakubwa wa watu wakatafuta kumwua.


Yoane alipata mamlaka ya kubatiza kutoka kwa nani? Kwa Mungu au kwa watu?” Nao wakaanza kupiga mafikiri pamoja na kusema: “Kama tukijibu kwamba mamlaka yake yalitoka kwa Mungu, atatuuliza: ‘Kwa sababu gani basi hamukumwamini?’


Wanafunzi wakaanza kusemezana hivi wao kwa wao: “Anasema hivi kwa sababu hatuna mikate.”


Yeye atasema, ‘Wewe ni baba yangu, Mungu wangu, mulima wa wokovu wangu.’


Uniombe nami nitakupa mataifa kuwa urizi wako, na dunia nzima kuwa mali yako.


Wakati siku za mavuno zilipotimia, akawatuma watumishi wake kwa wale walimaji kusudi wamupatie sehemu yake ya mavuno.


Halafu yule mwenye shamba akasema: ‘Nitafanya nini? Nitamutuma mwana wangu mupendwa; labda watamuheshimu.’


Halafu wakamukamata wakamwua na kutupa maiti yake inje ya shamba.” Kisha Yesu akauliza: “Basi yule mwenye shamba atawatendea walimaji wale namna gani?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite