Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 2:47 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

47 Na wote waliomusikia walishangaa kuona akili yake na majibu yake.

Gade chapit la Kopi




Luka 2:47
13 Referans Kwoze  

Yesu alipomaliza kusema maneno hayo, makundi ya watu wakashangaa sana kwa kuona namna alivyowafundisha;


Nao wakashangaa sana kuona namna alivyowafundisha, kwa maana aliwafundisha kama mutu mwenye mamlaka.


Ninaelewa kuliko walimu wangu wote, kwa sababu ninafikiri juu ya maagizo yako.


Wayuda wakashangaa, wakisema: “Mutu huyu amepata elimu kama hii namna gani, naye hakufundishwa?”


Watu waliomusikia walishangaa sana kuona namna alivyofundisha, kwa maana hakuwafundisha sawa na walimu wao wa Sheria, lakini kama mutu mwenye mamlaka.


Walinzi wakajibu: “Hatujasikia mutu akisema sawasawa na mutu yule!”


Nao wote wakamufurahia na kushangaa na maneno mazuri aliyosema. Wakasema: “Huyu si mwana wa Yosefu?”


na kwenda katika muji wake mwenyewe. Kule akaanza kuwafundisha watu katika nyumba zao za kuabudia, nao walishangaa na kuuliza: “Huyu amepata hekima na miujiza hii kutoka wapi?


Makundi ya watu waliposikia maneno hayo, wakashangaa sana na mafundisho yake.


Siku ya Sabato ilipotimia, akaanza kufundisha katika nyumba ya kuabudia. Watu wengi waliomusikiliza, wakashangaa sana na kuulizana: “Huyu amepata maneno haya yote kutoka wapi? Ni hekima ya namna gani aliyopata? Ni kwa uwezo wa namna gani anafanya miujiza kama hii?


Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walipopata habari hii, wakatafuta njia ya kumwua Yesu. Lakini walimwogopa, kwa sababu kundi lote la watu walishangaa na mafundisho yake.


Nyuma ya siku tatu, wakamukuta ndani ya hekalu, akiikaa katikati ya walimu wakubwa wa Sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maulizo.


Na wote waliosikia habari ile waliyoieleza wakashangaa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite