Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Basi Yosefu naye vilevile akaondoka katika muji Nazareti, wa jimbo la Galilaya, na kwenda Yudea katika muji wa kuzaliwa wa mufalme Daudi, unaoitwa Betelehemu. Alienda kule kwa sababu alikuwa mutu wa ukoo wa Daudi.

Gade chapit la Kopi




Luka 2:4
24 Referans Kwoze  

Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Maandiko Matakatifu hayakusema kwamba Kristo atazaliwa katika ukoo wa mufalme Daudi na katika muji Betelehemu, pahali Daudi alipoishi?”


Yawe akamwambia Samweli: “Utamulilia Saulo mpaka wakati gani? Wewe unajua kwamba mimi nimemukataa kuwa mufalme wa Israeli. Sasa, jaza ile pembe yako ya kuwekea mafuta, uondoke. Nitakutuma kwa Yese wa muji wa Betelehemu. Maana nimejipatia mufalme kati ya wana wake.”


Yesu akafika Nazareti, nafasi alipokomalia. Siku ya Sabato ilipotimia akaingia katika nyumba ya kuabudia kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama kwa kusoma Maandiko Matakatifu;


Kule akakaa katika muji ulioitwa Nazareti, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa mutu wa Nazareti.”


Baba yako akitambua kwamba siko, basi umwambie: ‘Daudi amenisihi nimupe ruhusa kusudi aende mbio katika muji wake Betelehemu, kuhuzuria kwa sadaka ya kila mwaka pamoja na jamaa yake’.


Wanawake wajirani wakatangaza jina wakisema: “Mutoto amezaliwa kwa Naomi”, nao wakamwita jina la Obedi. Kisha Obedi akamuzaa Yese aliyemuzaa Daudi.


Basi wazee waliokuwa kwenye mulango na watu wote waliokuwa pale wakajibu: “Ndiyo, sisi ni washuhuda. Yawe amufanye muke wako akuwe kama Rakeli na Lea, ambao wote wawili waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe upate kustawi katika jamaa ya Efurata, ukuwe na sifa katika Betelehemu.


Nyuma ya muda, Boazi akafika kutoka Betelehemu, akawasalimia wavunaji, akasema: “Yawe akuwe nanyi.” Nao wakamujibu: “Yawe akubariki.”


Natanaeli akamwuliza: “Kuna kitu kizuri kinachoweza kutoka Nazareti?” Filipo akamujibu: “Kuja uone.”


Saulo akamwuliza Daudi: “Kijana, wewe ni mwana wa nani?” Daudi akajibu: “Mimi ni mwana wa mutumishi wako Yese, kutoka muji wa Betelehemu.”


Daudi alikuwa mutoto wa Yese, wa ukoo wa Efurata kutoka Betelehemu katika inchi ya Yuda. Yese alikuwa na watoto wanane wa kiume. Wakati Saulo alipokuwa mufalme, yeye alikuwa amekwisha kuwa muzee, mutu mwenye umri mukubwa.


Samweli akafanya sawa alivyoambiwa na Yawe, akaenda Betelehemu. Wazee wa muji wakatoka kwenda kumupokea wakiwa wanatetemeka, wakamwuliza: “Umekuja kwa amani?”


Halafu wote wawili wakaendelea na safari mpaka Betelehemu. Walipofika kule, watu wote wakashangaa, hata wanawake wakaulizana: “Huyu ni Naomi?”


Ninaamua hivyo kwa sababu ya mama yako, Rakeli. Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani yeye alikufa katika inchi ya Kanana, tukiwa karibu kufika Efurata, akaniachia huzuni. Basi, nikamuzika palepale, kando ya njia inayokwenda Efurata, maana yake Betelehemu.”


Basi, Rakeli akakufa na kuzikwa kando ya njia inayokwenda Efurata, ni kusema Betelehemu.


Naye alipokuwa angali akifikiri juu ya maneno hayo, malaika wa Bwana akamutokea katika ndoto na kumwambia hivi: “Wewe Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumwoa muchumba wako Maria, kwa maana mimba yake imetokana na uwezo wa Roho Mutakatifu.


Watu wote walienda kujiandikisha, kila mumoja katika muji wake wa kuzaliwa.


Alienda kujiandikisha kule pamoja na muchumba wake Maria ambaye alikuwa mimba.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite