Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 2:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Na ilimutokea Simeoni kuingia ndani ya hekalu, akiongozwa na Roho. Wazazi walipomuleta mutoto wao Yesu kusudi wamutendee sawa ilivyoagizwa na Sheria,

Gade chapit la Kopi




Luka 2:27
15 Referans Kwoze  

Petro akiwa akifikiri juu ya maana ya yale maono, Roho Mutakatifu akamwambia: “Kuna watu watatu hapa wanaokutafuta.


Basi Yesu akarudia Nazareti pamoja nao, akaendelea kuwatii. Na mama yake alichunga maneno haya yote katika moyo wake.


Wazazi wake walipomwona, wakashangaa sana. Mama yake akamwuliza: “Mutoto wangu, kwa nini umetufanyia kama hivi? Mimi na baba yako tulikutafuta tukiwa na wasiwasi.”


Kila mwaka wazazi wa Yesu walikwenda Yerusalema kuhuzuria sikukuu ya Pasaka.


Nikashikwa na Roho wa Mungu, na malaika akanipeleka katika jangwa. Kule nikaona mwanamuke aliyekuwa akiikaa juu ya nyama mumoja wa ajabu mwekundu aliyeandikwa juu yake majina ya kumutukana Mungu. Nyama yule alikuwa na vichwa saba na pembe kumi.


Siku moja ya kumwabudu Bwana, nikashikwa na Roho wa Mungu, nikasikia sauti kubwa, inayolia kama baragumu,


Nao walipofika katika wilaya ya Misia, wakajaribu kwenda katika jimbo la Bitinia, lakini Roho wa Yesu hakuwaruhusu.


Naye Roho Mutakatifu akaniambia kwamba niende pamoja nao bila kusita. Na hawa wandugu sita munaowaona wakanisindikiza, nasi tukafika na kuingia sisi wote ndani ya nyumba ya Kornelio.


Roho Mutakatifu akamwambia Filipo: “Endelea, usogee karibu na lile gari.”


Yesu, akarudia toka kwenye muto Yordani, akijazwa na Roho, na Roho huyo akamwongoza kwenda katika jangwa.


Siku zilipotimia za Maria na Yosefu kutakaswa kama vile Sheria ya Musa inavyoagiza, wakamupeleka mutoto Yerusalema, kusudi wapate kumutolea kwa Bwana.


Kisha Roho Mutakatifu akamwongoza Yesu kwenda katika jangwa kusudi ajaribiwe na Shetani.


Kisha, nikakamata ile barua ya ununuzi niliyoipiga muhuri, ambayo ilikuwa na masharti na kanuni, pamoja na barua ingine iliyokuwa wazi.


Simeoni akamupokea katika mikono, akamushukuru Mungu, akisema:


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite