Watumishi wa mufalme wakamwambia Akisi: “Huyu si Daudi, mufalme wa inchi ya Israeli? Si huyu ambaye walikuwa wakiimbiana juu yake katika ngoma, wakisema: ‘Saulo ameua maelfu yake na Daudi ameua elfu makumi yake?’ ”
Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.
Huu ndio mwisho wa jambo hilo. Mawazo yangu yaliniogopesha sana mimi Danieli, hata rangi yangu ikabadilika. Lakini nilichunga jambo hilo ndani ya moyo wangu.