Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Na hiki ndicho kitambulisho kwenu: mutamukuta mutoto muchanga amefunikwa nguo za kitoto, naye amelalishwa katika sanduku ya kukulishia nyama.”

Gade chapit la Kopi




Luka 2:12
11 Referans Kwoze  

Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Umwombe Yawe, Mungu wako, akupe kitambulisho; kikuwe ni kutoka chini kuzimu au juu mbinguni.


Walikulilia wewe, wakaokolewa; walikutegemea, nao hawakufezeheka.


Hezekia akamwuliza Isaya: “Ni kitambulisho gani ambacho kitanionyesha kwamba kweli Yawe ataniponyesha na katika siku ya tatu nitaweza kwenda kwa nyumba ya Yawe?”


“Na hiki ndicho kitakuwa kitambulisho kwako Hezekia: Mwaka huu na mwaka unaokuja mutakula kinachoota chenyewe bila kupandwa. Lakini katika mwaka wa tatu mutapanda na kuvuna mavuno; mutapanda mizabibu na kula matunda yake.


Na litakalowapata watoto wako wawili, Hofuni na Finehasi, ni hili: Wote wawili watakufa siku moja. Hiki kitakuwa ni kitambulisho kwako.


Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”


Akazaa mwana, ndiye muzaliwa wake wa kwanza. Akamufunika nguo za kitoto na kumulalisha katika sanduku ya kukulishia nyama, kwa sababu walikosa nafasi ya kukaa katika nyumba ya kupangisha wageni.


Mara moja kukaonekana kundi kubwa la wamalaika kutoka mbinguni wakiwa pamoja na yule malaika, wakimutukuza Mungu na kusema:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite