Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 19:42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

42 akisema: “Kama wewe vilevile ungejua leo hii kitu kinachoweza kukuletea amani! Lakini sasa kitu hicho kimefichwa, nawe hauwezi kukiona!

Gade chapit la Kopi




Luka 19:42
35 Referans Kwoze  

Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa, wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwa namna gani.


Maandiko Matakatifu yanasema: “Leo ikiwa munasikiliza sauti ya Mungu, musifanye mioyo yenu kuwa migumu kama babu zenu walivyofanya wakati walipomwasi Mungu.”


Ingekuwa heri ungalizitii amri zangu! Halafu baraka zingekutiririkia kama muto, ungefanikiwa kwa wingi kama mawimbi ya bahari.


Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.


Mumutafute Yawe wakati angali anaweza kupatikana, mumwombe musaada wakati angali karibu.


Lakini muonyane kila siku kwa muda wote ambao lile neno “leo” linalotajwa lingali linatuelekea kusudi hata mumoja wenu asikuwe mugumu kwa kudanganywa na zambi.


Watakuharibu kabisa pamoja na wakaaji wako. Hawatakuachia hata jengo moja lisilobomolewa kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuja kukuokoa.”


Halafu Paulo na Barnaba wakawaambia bila woga: “Ilitupasa kwanza kuhubiri Neno la Mungu kwenu. Lakini kwa kuona mumelikataa na kujihesabu ninyi wenyewe kwamba uzima wa milele haufai kwenu, basi tunashugulika na watu wa mataifa mengine.


Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?


Watu hao hawajui wala hawaelewi kitu chochote. Wamefungwa macho wasipate kuona na akili wasipate kufahamu.


Kwa hiyo, kama vile Roho Mutakatifu anavyosema: “Leo ikiwa munasikiliza sauti ya Mungu,


Hivyo, nikawaacha wabaki katika ugumu; wafuate mashauri yao wenyewe.


Kwa hiyo, kila mwaminifu akutolee maombi wakati wa taabu. Mafuriko ya maji hayatamufikia.


Heri wangekuwa siku zote na mawazo kama haya wakiniheshimu na kushika amri zangu! Mambo yao yote yangewaendekea vizuri, wao wenyewe na wazao wao milele.


Na kama musiponisikiliza, moyo wangu utalia machozi kwenye uficho, kwa sababu ya kiburi chenu. Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi, maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.


Yesu alipokaribia muji wa Yerusalema, na alipouona, akaulilia,


Kwa maana siku zitakufikia wakati waadui zako watakapokuzunguka kwa vita, watakapojenga ukuta wa kujikingia pembeni yako, na kukusonga pande zote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite