Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 19:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Kisha kusema maneno hayo, Yesu akatembea mbele ya kundi la watu kwenda Yerusalema.

Gade chapit la Kopi




Luka 19:28
9 Referans Kwoze  

Siku za Yesu za kunyanyuliwa mbinguni zikakaribia. Kwa hiyo akakusudia sana kwenda Yerusalema,


Kristo aliteswa kimwili. Basi ninyi vilevile mujikaze mupate kuwa na nia kama ile yake. Kwa maana mutu anayevumilia mateso ya mwili, anaachana kabisa na zambi.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Halafu Yesu akawatwaa wanafunzi wake kumi na wawili pembeni, akawaambia: “Tunapanda kwenda Yerusalema, na maneno yote yaliyoandikwa na manabii juu ya Mwana wa Mutu yatatimizwa.


Niko na muzigo wa mateso ninaopaswa kubeba, nami ninasongwa sana mpaka mapaswa hayo yatakapotimizwa!


Lakini Yesu akamwambia Petro: “Rudisha upanga wako katika kifuko chake! Inanipasa kunywa kikombe cha mateso Baba yangu alichonitayarishia.”


Yesu akajibu akimwelezea: “Mutu mumoja alitoka Yerusalema akishuka kwenda Yeriko. Alipokuwa katika njia, akashambuliwa na wanyanganyi, wakamuvua nguo, wakamupigapiga, wakajiendea, wakimwacha karibu kufa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite