Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 18:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Maana atatolewa katika mikono ya watu wa mataifa mengine. Watamuchekelea, watamutukana na kumutemea mate.

Gade chapit la Kopi




Luka 18:32
26 Referans Kwoze  

Basi Herode na waaskari wake wakamuchekelea Yesu na kumuzarau. Wakamuvalisha nguo zinazokuwa sawa za mufalme na kumurudisha kwa Pilato.


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Wale walionipiga, niliwaelekezea mugongo wangu, wale walioziongoa ndevu zangu, mashavu yangu. Sikuficha uso wangu wakati watu waliponitukana na kunitemea mate.


Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.


Wengine katikati yao wakaanza kumutemea Yesu mate, wakamufunika uso na kumupiga ngumi, wakimwambia: “Tambua sasa ni nani aliyekupiga!” Nao waaskari walinzi wakamukamata Yesu na kumupiga makofi.


Halafu wamoja wakamutemea mate juu ya uso, na kumupiga ngumi. Na wengine wakamupiga makofi,


Tangia wakati ule Yesu akaanza kuwaambia wanafunzi wake waziwazi kwamba ni sherti kwake kwenda Yerusalema, ateswe kule na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, auawe, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.


Yawe anasema hivi: Lakini wewe Betelehemu katika Efurata, wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda, lakini kwako kutanitokea mutawala atakayetawala juu ya Israeli. Asili yake ni ya zamani sana.


Wengi waliomwona walishituka, kwa vile sura yake ilikuwa imeharibika; hakukuwa tena na umbo la mwanadamu!


Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.


Pilato akajibu: “Mimi si Muyuda. Watu wa taifa lako na wakubwa wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?”


Nao wakamujibu: “Kama asingekuwa mutenda maovu, tusingemuleta kwako.”


Yesu aliposema maneno haya, mumoja wa walinzi waliokuwa karibu naye, akamupiga kofi, akisema: “Ni hivi unavyopaswa kumujibu Kuhani Mukubwa?”


Watu walisimama pale wakiangalia. Nao wakubwa wa Wayuda walimusimanga Yesu, wakisema: “Aliokoa watu wengine, sasa ajiokoe yeye mwenyewe ikiwa yeye ndiye Masiya, yule aliyechaguliwa na Mungu.”


Kisha watu wote wa Baraza Kubwa wakasimama, wakamupeleka Yesu mbele ya Pilato.


Wakamufunga, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa liwali Pilato.


Na kulipokucha asubui mapema, wakamutosha Yesu kwa Kayafa na kumupeleka kwenye nyumba ya liwali. Lakini Wayuda wenyewe hawakuingia ndani ya nyumba ya liwali, kwa maana kwa njia ile wangejichafua na kutoweza kuwa tayari kula karamu ya Pasaka.


Asubui mapema, mara moja wakubwa wa makuhani wakafanya shauri pamoja na wasimamizi wa watu, walimu wa Sheria na wakubwa wote wa baraza. Wakamufunga Yesu, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa Pilato.


na kumutoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine. Nao watamuchekelea, watamupiga fimbo na kumutundika juu ya musalaba. Lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”


na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatesa na kuwaua.


Watamupiga fimbo na kisha watamwua. Lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake atafufuka!”


(Ilifanyika hivi kusudi litimie lile neno Yesu alilosema kwa kuonyesha kifo gani atakachokufa.)


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite