Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 18:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 atapokea mara mingi zaidi katika wakati wa sasa. Na katika wakati utakaokuja atapokea uzima wa milele.”

Gade chapit la Kopi




Luka 18:30
19 Referans Kwoze  

Nyuma ya Yobu kuwaombea warafiki zake, Yawe akamurudishia Yobu hali yake ya kwanza. Akamupa mara mbili ya yote aliyokuwa nayo pale mbele.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa! “Yule atakayeshinda, nitamupa ile mana iliyofichwa. Na nitamupa vilevile jiwe dogo jeupe, na juu yake kumeandikwa jina jipya ambalo hakuna mutu yeyote anayelijua, isipokuwa tu yule anayelipewa.


Kila mutu anayesema vibaya juu ya Mwana wa Mutu atasamehewa, lakini kila mutu anayesema vibaya juu ya Roho Mutakatifu, hatasamehewa katika ulimwengu huu, wala katika ule unaokuja.


Hakika, dini ni pato kubwa kwa mutu kama anafurahia vitu anavyokuwa navyo.


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


Ninafurahi kwa sababu ya neno lako, kama mutu aliyekuta kitu cha bei kali.


Kweli, ninapenda amri zako, kuliko hata zahabu safi kabisa.


Maagizo yako ni urizi mukubwa kwangu milele; hayo ni furaha ya moyo wangu.


Maagizo yako ni matamu sana kwangu; ni matamu kuliko asali!


Sheria uliyoweka ni bora kwangu, kuliko mali zote za dunia.


Afazali mali kidogo ya mutu wa haki kuliko utajiri mwingi wa watu waovu.


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite