27 Yesu akajibu: “Mambo yasiyoweza kutendeka kwa uwezo wa mwanadamu yanawezekana kwa Mungu.”
Ee Bwana wangu Yawe, ni wewe ambaye kwa nguvu zako nyingi na uwezo wako mukubwa, umeziumba mbingu na dunia.
Yesu akawaangalia na kuwaambia: “Jambo hilo haliwezi kutendeka kwa uwezo wa mwanadamu, lakini kwa uwezo wa Mungu, yote yanawezekana.”
Kwa maana hakuna kisichowezekana kwa Mungu.”
Ninajua kwamba unaweza kila kitu, lolote unalokusudia haliwezi kuzuiliwa.
Kuna jambo lolote lisilowezekana kwa Yawe? Nitakurudilia wakati uliopangwa, kwa wakati kama huu katika mwaka, na Sara atakuwa na mutoto mwanaume.”
Yawe wa majeshi anasema hivi: Kwa watu hawa waliobaki, hali hii inaonekana kuwa kitu kisichowezekana; lakini munazani haiwezekani kwangu mimi? –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.
Nao waliosikia maneno haya wakasema: “Ni nani basi anayeweza kuokolewa?”