Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 18:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Yesu akamwuliza: “Sababu gani unaniita mwema? Hakuna mutu anayekuwa mwema isipokuwa Mungu peke yake.

Gade chapit la Kopi




Luka 18:19
10 Referans Kwoze  

Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?


Nani anayeweza kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu? Hakuna anayeweza.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, inaonyesha hakika kwamba Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa Roho Mutakatifu wale wanaomwomba kwake.”


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Mutawala mumoja akamwuliza Yesu: “Mwalimu mwema, nifanye nini kusudi nipate uzima wa milele?”


Unajua jinsi amri zinavyosema kwamba: ‘Usizini, usiue, usiibe, usishuhudie uongo, uwaheshimu baba yako na mama yako.’ ”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite