Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 18:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Ninafunga kula chakula mara mbili kila juma na ninatoa fungu moja la kumi la vitu vyote ninavyopata.’

Gade chapit la Kopi




Luka 18:12
24 Referans Kwoze  

“Ole kwenu, ninyi Wafarisayo! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula na kila namna ya mboga; lakini mumezarau haki na upendo wa Mungu. Mambo hayo ndiyo mulipaswa kushika pasipo kuacha mengine.


Wanafunzi wa Yoane Mubatizaji wakamufikia Yesu na kumwuliza: “Sababu gani sisi na Wafarisayo tunafunga kula chakula, lakini wanafunzi wako hawafungi?”


Na ni hivi inavyokuwa kwenu vilevile. Wakati mutakapokwisha kufanya yote muliyoamuriwa, museme: ‘Sisi ni watumishi tu, tumetimiza tu mapaswa yetu.’ ”


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


“Mujiangalie musifanye matendo mema mbele ya watu kusudi mujionyeshe kwao. Kwa maana mukifanya hivi hamutapata faida kutoka kwa Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Ninawajibia hivi: Ni sawa kwa mutu kumudanganya Mungu? Hapana! Lakini ninyi munanidanganya! Ingawa hivyo ninyi munauliza: Tunakudanganya kwa namna gani? Kweli! Munanidanganya juu ya zaka na sadaka zenu.


Si kwa matendo yenu, kusudi mutu asipate kujivuna.


Nami niliendelea vizuri sana katika dini ya Kiyuda kuwapita watu wote wengine wa kabila langu wenye umri wangu, nikijikaza sana kushika desturi za babu zetu.


Alifanya vile kusudi hata mutu mumoja asijivune mbele yake.


Basi sasa mutu ataweza kujivuna? Hapana! Kwa sababu gani? Kwa sababu anatii Sheria? Hapana. Lakini kwa sababu anamwamini Yesu.


“Munapofunga kula chakula, musifanye kama wanafiki, wanaojigeuza kuwa wenye sikitiko na kukunja nyuso zao, kusudi watu waone kwamba wanafunga. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


“Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Akamwambia: “Fuatana nami kusudi ujionee jinsi ninavyokuwa mwaminifu kwa Yawe.” Basi, wakasafiri pamoja katika gari lake.


Samweli alipomufikia Saulo, Saulo akamwambia Samweli: “Yawe akubariki! Nimetimiza amri ya Yawe.”


Mungu akakutana naye. Balamu akamwambia: Nimetayarisha mazabahu saba na kutoa ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja juu ya kila mazabahu.


kwa sababu sehemu ya kumi Waisraeli wanayonitolea nimewapa kuwa urizi wao. Ndiyo maana nimesema kwamba wao hawatakuwa na urizi kati ya Waisraeli.


Basi ninawaambia: musipokuwa wenye haki kuliko walimu wa Sheria na Wafarisayo hamutapokelewa katika Ufalme wa mbinguni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite