Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 18:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu kwa kuwaonyesha kwamba wanapaswa kuomba siku zote pasipo kuchoka.

Gade chapit la Kopi




Luka 18:1
26 Referans Kwoze  

Mudumu katika kuomba. Munapoomba mukeshe na kumutolea Mungu shukrani.


Mufurahi mukiwa na tumaini, muvumilie katika mateso, mudumu katika kuomba.


Musijisumbue juu ya neno lolote, lakini katika kila neno mutoe mahitaji yenu kwa Mungu, mukimwomba, mukimusihi na kumushukuru.


Mumwombe Mungu kila wakati mukiongozwa na Roho. Mumwombe na kumusihi kwa kila namna. Kwa hiyo mukeshe bila kuchoka mukiwaombea watu wote wa Mungu.


Kwa hiyo mutakapokuja kunililia na kuniomba, nitawasikiliza.


Basi mukeshe na kuomba kila wakati, kusudi mupate nguvu ya kuepuka mambo hayo yote yatakayotokea, nanyi mupate kuweza kusimama mbele ya Mwana wa Mutu.”


Tusichoke kutenda mema; kwa maana siku zitakapotimia tutavuna kama tusiporegea.


Wewe ni Mungu wangu; basi, unionee huruma, maana ninakulilia muchana kutwa.


Yawe atajenga upya Sayuni, na kuonyesha utukufu wake.


Kwa wema wake, Mungu ametupatia utumishi huu, na kwa sababu hii sisi hatukati tumaini.


Mwanainchi mwenzenu Epafra anawasalimia vilevile. Yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, hachoki kwa kuwaombea ninyi, kusudi musimame imara mukikomaa kiroho na kuwa tayari kwa kutimiza kabisa mapenzi ya Mungu.


Niliteremuka mpaka kwenye misingi ya milima, katika inchi ambayo milango yake imefungwa milele. Lakini wewe, ee Yawe, Mungu wangu, umenipandisha nikiwa muzima kutoka mule ndani ya shimo.


Ee Mungu, unastahili sifa huko Sayuni. Watu wanapaswa kukutimizia viapo vyao,


Ninaamini kwamba nitauona uzuri wa Yawe katika makao ya wazima.


Lakini wote wanaomutumainia Yawe, watapata nguvu mupya. Watapanda juu kwa mabawa kama tai, watakimbia bila kuchoka, watatembea bila kuregea.


musimupe hata nafasi ya kupumzika, mpaka atakapousimika Yerusalema, na kuufanya kuwa wenye sifa katika ulimwengu wote.


Hana aliendelea kumwomba Yawe kwa muda murefu, na kuhani Eli akakuwa anaangalia midomo yake.


Kwa maana kila mutu anayeomba anapewa; anayetafuta anapata, anayepiga hodi anafunguliwa mulango.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite