Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 17:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kwa sababu hii mujiangalie vizuri. “Kama ndugu yako akikosa, umwonye, na akigeuka toka katika zambi zake, umusamehe.

Gade chapit la Kopi




Luka 17:3
18 Referans Kwoze  

Usimuchukie ndugu yako ndani ya moyo wako, lakini upatane siku zote na mwenzako kusudi usitende zambi.


Kisha Petro akamwendea Yesu na kumwuliza: “Bwana, ndugu yangu akiendelea kunikosea, nitamusamehe mpaka mara ngapi? Mara saba inatosha?”


Usimwonye mwenye kiburi maana atakuchukia; umwonye mwenye hekima naye atakupenda.


Wandugu zangu, mutu mumoja kati yenu akipotea mbali na ukweli, na mutu mwingine akimurudisha,


Afazali mutu anayekuonya waziwazi, kuliko yule anayeficha upendo.


Mufanye angalisho sana kusudi musisahau agano ambalo Yawe, Mungu wenu, amefanya nanyi. Musijifanyie sanamu ya kuchonga katika umbo la kitu chochote ambacho Yawe, Mungu wenu, amewakataza kumufananisha nacho,


“Lakini mukuwe waangalifu na kufanya angalisho sana kusudi musisahau mambo yale muliyoona kwa macho yenu wenyewe, kusudi isitokee hata mara moja katika maisha yenu mambo hayo kusahaulika ndani ya mioyo yenu. Muwaelezee watoto wenu na wajukuu wenu


Mufanye angalisho musifanye agano na wakaaji wa inchi munayoiendea, maana hiyo itakuwa mutego kati yenu.


Basi, mujiangalie wenyewe, kusudi musipoteze matunda ya kazi yenu, lakini mupokee zawadi kamili.


Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.


Muangalie vizuri mwenendo wenu. Musiishi kama wajinga lakini muishi kama wenye hekima.


“Mujilinde vizuri, kusudi musilemewe na kutafuta kula ulafi, kulewa na kusumbukia maisha. Kama si vile, Siku ile ya kurudia kwa Kristo itawafikia kwa rafla


Onyo kwa mwenye akili lina maana, kuliko mapigo mia moja kwa mupumbafu.


Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.


“Kwa hiyo mukuwe waangalifu kusudi musisahau kwamba Yawe aliposema nanyi kule kwenye milima ya Horebu katikati ya moto hamukumwona kwa umbo. Kwa sababu hiyo mufanye angalisho sana,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite