Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 16:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Basi kama ninyi hamukukuwa waaminifu kwa kulinda mali ya dunia hii, ni nani atakayeweza kuwatumainia kwa kulinda mali ya kweli?

Gade chapit la Kopi




Luka 16:11
9 Referans Kwoze  

Muuzishe vitu munavyokuwa navyo, muwasaidie wamasikini. Mujiwekee feza zisizoweza kuwa na upungufu, nayo akiba isiyoweza kumalizika katika mbingu. Kule wizi hawawezi kukaribia wala nondo hawaharibu.


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


Mimi ni mudogo kuliko watu wote wa Mungu, lakini Mungu amenijalia neema ya kutangaza kwa watu wa mataifa mengine Habari Njema ya baraka za Kristo zisizoweza kuhesabiwa.


Yesu aliposikia maneno haya, akamwambia: “Ungali unakosewa na kitu kimoja tu: uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudie unifuate!”


Yesu akaongeza kusema: “Nami ninawaambia: mutumie mali ya dunia hii kwa kuunga urafiki, kusudi wakati mali ile itakapokosekana, mupate kupokelewa kwenye makao ya milele.


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.


Na kama hamuwezi kulinda mali ya mutu mwingine kwa uaminifu, ni nani atakayewapa mali yenu ya pekee?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite