Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 15:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Atakapomwona, atamubeba kwa furaha juu ya mabega.

Gade chapit la Kopi




Luka 15:5
31 Referans Kwoze  

Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Yesu akamwambia: “Leo nyumba hii imeokolewa, kwa sababu mutu huyu vilevile ni wa uzao wa Abrahamu.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Yesu akamujibu: “Kweli ninakuambia wewe: leo hii utakuwa pamoja nami katika Paradizo.”


Kwa hivi ilitupasa kushangilia na kufurahi, kwa maana mudogo wako huyu alikuwa amekufa na amefufuka, alikuwa amepotea na sasa ameonekana.’ ”


Basi, ninafurahia kufa kwa mutu mwovu? Hapana! Mimi ninapendelea aachane na njia zake mbaya apate kuishi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Ninyi ambao kwa imani munalindwa salama kwa nguvu za Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa kwa mwisho wa nyakati.


Kwa njia hiyo wanaweza tena kupata ufahamu na kuponyoka katika mitego ya Shetani, aliyewanasa na kuwafanya watimize mapenzi yake.


Kwa maana tulipohubiri Habari Njema kwenu, hatukuihubiri kwa maneno tu, lakini kwa uwezo na kwa musaada wa Roho Mutakatifu na kwa uhakika kabisa. Munajua namna gani tulivyoishi katikati yenu, kusudi tupate kuwafalia.


Nimewekwa kuwa mutumishi wa Habari Njema kwa njia ya zawadi Mungu aliyonipatia kutokana na uwezo wake.


Kwa maana sisi ni viumbe vya Mungu, na kwa kuungana kwetu na Yesu Kristo, alituumba kusudi tuishi maisha ya matendo mema, ambayo Mungu alitutayarishia tangu mbele tupate kuyatenda.


“Nimewaambia ninyi maneno haya kusudi mufurahi sawa mimi, na furaha yenu ikuwe kubwa kabisa.


Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,


Yeye ndiye atakayeleta amani. Waasuria wakishambulia inchi yetu, na kuingia katika nyumba zetu nzuri, tutatuma walinzi wetu wapigane nao, tutawapeleka waongozi wetu kwa wingi.


Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Ninyi mutaitwa: Watu Watakatifu, Watu waliokombolewa na Yawe. Nawe Yerusalema utaitwa: Muji Mungu anaoupenda, Muji ambao Mungu hakuuacha.


Maana kama vile kijana mwanaume anavyomwoa binti, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi anavyofurahi juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.


“Ni nani kati yenu akiwa na kondoo mia moja, na mumoja wao akipotea, atakayekosa kuwaacha wale wengine makumi tisa na tisa kwenye mashamba ya kulishia wanyama na kwenda kumutafuta yule aliyepotea mpaka atakapomupata?


Naye anaporudia kwake, atawaita warafiki na jirani zake na kuwaambia: ‘Mufurahi pamoja nami, kwa sababu nimemupata kondoo wangu aliyepotea!’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite