Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 15:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 “Ni nani kati yenu akiwa na kondoo mia moja, na mumoja wao akipotea, atakayekosa kuwaacha wale wengine makumi tisa na tisa kwenye mashamba ya kulishia wanyama na kwenda kumutafuta yule aliyepotea mpaka atakapomupata?

Gade chapit la Kopi




Luka 15:4
19 Referans Kwoze  

Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.


Kwa maana Mwana wa Mutu alikuja kutafuta na kuokoa yule aliyepotea.”


Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.


Yesu akawajibu: “Kama mutu mumoja kati yenu akiwa na kondoo mumoja, na kondoo yule akitumbukia ndani ya shimo kwa siku ya Sabato, hatamukamata na kumwondosha mule siku ile ile?


Nanyi, ee kondoo wangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Ninatangatanga kama kondoo aliyepotea; ukuje kunitafuta mimi mutumishi wako, maana sikusahau amri zako.


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


Watu wangu walikuwa kama kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha, wakawageuza kuelekea kwenye milima; walitembea toka mulima mpaka kilima, wakasahau makao yao.


Lakini Bwana akamujibu: “Ninyi wanafiki! Kuna mutu mumoja kati yenu anayekosa kumufungua ngombe au punda wake toka katika upango kwa siku ya Sabato kwa kumupeleka kunywa maji?


Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– nimechoka kuwaona kondoo wangu wamekuwa chakula cha nyama wakali kwa vile hakukukuwa muchungaji; wachungaji wangu hawakuwatafuta kondoo wangu, lakini wamejikulisha wao wenyewe pahali pa kuwakulisha kondoo wangu.


Wewe unayemuhukumu mwingine hauna namna yoyote ya kujitetea, haizuru wewe ni nani. Kwa maana wakati unapohukumu mwingine, unajikatia hukumu wewe mwenyewe, kwa sababu wewe unayehukumu unatenda mambo yale yale.


Katika miji ya inchi yenye milima, katika miji ya Shefela na katika miji ya jangwa la Negebu, katika inchi ya Benjamina, kandokando ya Yerusalema na katika miji ya Yuda, watu watahesabu tena kondoo wao. –Ni Yawe anayesema.


Wanaokuwa zaifu hamukuwatia nguvu, wagonjwa hamukuwatunza, waliovunjika hamukuwafunga kwa kitambaa, waliotangatanga hamukuwarudisha na waliopotea hamukuwatafuta. Lakini mukawatawala kwa kinguvu na kuwatesa.


Halafu Yesu akawaambia mufano huu:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite