Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 15:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Kisha akafunga safari yake na kurudia kwa baba yake. “Alipokuwa angali mbali kidogo, baba yake akamwona, akamusikilia huruma. Akamukimbilia, akamukumbatia mwana wake na kumubusu.

Gade chapit la Kopi




Luka 15:20
22 Referans Kwoze  

Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.


Lakini sasa, katika kuungana kwenu na Yesu Kristo, ninyi muliokuwa mbali, mumekuwa karibu kwa njia ya damu ya Kristo.


Lakini Yawe anasema: Munafikiri kwamba mama anaweza kumusahau mutoto anayemunyonyesha, wala kumuchukia mutoto wa tumbo lake? Hata kama mama anaweza kumusahau mutoto wake, mimi sitakusahau hata kidogo.


Basi, Esau akakwenda mbio kumupokea Yakobo, akamukumbatia, kumubusu kwenye shingo, na wote wawili wakalia.


Hivi, Kristo amekuja kutangaza Habari Njema ya amani kwa ninyi watu wa mataifa mengine, muliokuwa mbali na Mungu, na kwa Wayuda waliokuwa karibu naye.


Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Niliona mwenendo wao, lakini nitawaponyesha; nitawaongoza na kuwapa faraja, nitawatuliza hao wanaoomboleza.


Yosefu akapanda gari lake la farasi, akakwenda kumupokea baba yake Israeli, kule Goseni. Alipomufikia baba yake, alimukumbatia na kulia kwa kitambo kirefu.


Kisha Yosefu akamukumbatia Benjamina, ndugu yake, akalia. Benjamina naye akalia, wakiwa wanakumbatiana.


Na wote walilia sana wakimukumbatia na kumubusu.


Kwa maana ahadi hii ya Mungu ilitolewa kwenu, kwa watoto wenu na kwa wote wanaokaa mbali, ndio wote ambao Bwana Mungu wetu atakaowaita.”


Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.


Kwa hiyo Yoabu akaenda na kumwelezea mufalme maneno hayo yote, naye akamwita Abusaloma. Abusaloma akaingia kwa mufalme, akaanguka uso mpaka chini mbele ya mufalme. Na mufalme akamubusu Abusaloma.


Sababu hii sistahili kuhesabiwa tena sawa vile mwana wako; unihesabu sawa vile mumoja wa watumishi wako.’


Mwana wake akamwambia: ‘Baba, nimemukosea Mungu na nimekukosea wewe vilevile. Sababu hii sistahili kuhesabiwa tena sawa vile mwana wako.’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite