Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 15:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Nyuma ya siku chache, yule mudogo akauzisha urizi wake na kwenda katika inchi ya mbali. Kule aliponda mali yake yote katika maisha ya ovyo.

Gade chapit la Kopi




Luka 15:13
35 Referans Kwoze  

Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?


Anayependa hekima anamufurahisha baba yake; lakini anayeandamana na kahaba anapoteza mali yake.


Anayependa raha atakuwa masikini; anayefikiria tu kula na kunywa hatatajirika.


Mutoto anayeshika sheria ni mwenye hekima, lakini rafiki wa walafi anafezehesha baba yake.


“Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyezoea kuvaa nguo zenye kuwa laini sana za bei kali zaidi na aliyeishi katika raha siku zote.


Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu: “Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyekuwa na mulinzi wa mali yake. Yule mulinzi akachongewa kwa bwana wake kwamba anaponda mali yake.


Lakini mwana wako huyu aliyeharibu mali yako katika ukahaba alipofika, ukamuchinjia yule ngombe mwenye kunona!’


Anasema hivi: Enyi watu wangu, nimewatendea nini? Nimewachokesha kwa kitu gani? Munijibu!


Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!


Watu wangu wametenda maovu mawili; wameniacha mimi ninayekuwa chemichemi ya maji ya uzima, wakajichimbia visima vyao wenyewe, visima vyenye nyufa, visivyoweza kuchunga maji.


Wao wanaambiana hivi: Mukuje, tuende kutafuta divai; mukuje tukunywe tushibe kinywaji kikali! Kesho itakuwa kama leo, tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.


Mugeuke na kuiacha njia ya ukweli; musituambie tena juu ya Mungu, Mutakatifu wa Israeli.


Lakini ninyi mukafurahi na kusherehekea. Mulichinja ngombe na kondoo, mukakula nyama na kunywa divai. Ninyi mulisema: Acha tukule na kunywa maana kesho tutakufa.


Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.


Mutu aliyepotea mbali na kwake ni kama ndege aliyepotea mbali na chicha yake.


Katika nyumba ya mwenye hekima kuna hazina za bei kali, lakini mupumbafu anaponda mali yake yote.


Mutu muvivu katika kazi yake ni ndugu ya muharibifu.


Mutu anapoteza kipande cha mukate kwa kahaba, lakini mwanamuke muzinzi atapoteza uzima wako wote.


Anayejitenga nawe, hakika ataangamia. Anayekukana, utamwangamiza.


Watalipwa mateso kwa sababu ya mateso waliyoleta. Wanafurahia kutimiza waziwazi tamaa zao mbaya za kimwili muchana kati. Kufika kwao katika karamu zenu kunaleta haya na chukizo kubwa wanapofurahia mambo yao ya udanganyifu.


Hivi, Kristo amekuja kutangaza Habari Njema ya amani kwa ninyi watu wa mataifa mengine, muliokuwa mbali na Mungu, na kwa Wayuda waliokuwa karibu naye.


Lakini sasa, katika kuungana kwenu na Yesu Kristo, ninyi muliokuwa mbali, mumekuwa karibu kwa njia ya damu ya Kristo.


Yule mudogo akamwambia baba yake: ‘Baba, unipe ile sehemu ya urizi inayopaswa kuwa yangu.’ Basi baba akagawanya mali yake kati ya wana wake wote wawili.


Alipokwisha kumaliza mali yake yote, njaa kubwa ikatokea katika inchi ile, akaanza kuishi katika ukosefu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite