6 Nao hawakuweza kumujibu neno.
Na hakuna mutu aliyesubutu tena kumwuliza maneno mengine.
lakini hawakuweza kumushinda kwa sababu ya hekima yake na kwa sababu ya Roho Mutakatifu aliyemwongoza kusema.
Kwa maana mimi mwenyewe nitawapa masemi na hekima hata waadui zenu hawataweza kuyapinga wala kuyakataa.
Basi watu wale hawakuweza kumunasa katika neno lolote mbele ya watu, lakini wakashangaa na jibu lake, nao wakanyamaza.
Yesu aliposema vile, wapinzani wake wote wakafezeheka, lakini kundi lote la watu wote walifurahia matendo yote ya ajabu aliyoyatenda.
Basi hakuna mutu aliyeweza kumujibu neno, na tangia siku ile hakuna aliyesubutu kumwuliza tena neno.