Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 14:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Basi yule mutumishi akarudia na kumwelezea bwana wake maneno hayo yote. Halafu bwana wa nyumba akakasirika, na kumwambia: ‘Kwenda upesi katika nafasi za mukutano na katika barabara za muji, uwalete wamasikini, vilema, vipofu na viwete na kuwaingiza humu.’

Gade chapit la Kopi




Luka 14:21
38 Referans Kwoze  

Lakini wakati unapofanya karamu, uwaalike wamasikini, vilema, viwete na vipofu.


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.


Kisha Yesu akasema: “Nimekuja katika dunia kusudi hukumu ipate kufanyika; maana yake vipofu wapate kuona, nao wanaoona wapate kuwa vipofu.”


Kwa maana ninawaambia kwamba kati ya wale niliokuwa nimewaalika, hakuna hata mumoja wao atakayeonja vyakula vya karamu yangu.’ ”


Viwete watarukaruka kama paa, na bubu wataimba kwa furaha. Maji yatabubujika katika jangwa na vijito katika mbuga.


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


Anawainua wazaifu toka katika mavumbi, anawanyanyua wakosefu toka katika majivu, na kuwaikalisha pamoja na wakubwa, na kuwarizisha viti vya heshima. Maana, minara ya dunia ni ya Yawe; yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


Ndani ya kinywa chake mulitoka upanga mukali kwa kushinda mataifa. Naye atatawala kwa fimbo ya chuma na kukamua zabibu ndani ya kikamulio cha divai kinachojaa kasirani kali ya Mungu Mwenye Uwezo.


Mutii waongozi wenu na kushika maagizo yao. Kwa maana wao wanashugulika kila mara kwa ajili ya roho zenu, na wao wanapaswa kutoa habari ya kazi yao mbele ya Mungu. Kwa kufanya vile mutawaruhusu kufanya kazi yao kwa furaha wala si kwa huzuni, kwa maana haitawafalia kitu kama wakitumika katika huzuni.


Iliandikwa vilevile kwamba kwa jina lake watahubiri mataifa yote, kuanzia Yerusalema, kusudi wageuke toka katika zambi na wapate kusamehewa.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


Ewe Sayuni, kamba zako zimeregea, haziwezi kushikilia matanga yake, wala kufungia paa zao. Lakini vitu vingi vilivyonyanganywa vitagawanywa; hata vilema wataweza kupata sehemu yao.


Mitume waliporudia toka kuhubiri wakamwelezea Yesu mambo yote waliyofanya. Kisha akaondoka pamoja nao na kwenda kwenye nafasi ya upekee karibu na muji Betesaida.


Nao watumishi wenzake walipoona jambo hilo, wakahuzunika sana, wakaenda kumwelezea bwana wao yote yaliyotokea.


Halafu wanafunzi wakamufikia na kumwuliza: “Unajua kwamba Wafarisayo walikwazwa kwa kusikia maneno hayo uliyosema?”


Na agano hilo likavunjwa siku ileile. Wale wachuuzi wa kondoo waliokuwa wananiangalia, wakajua kwamba neno la Yawe lilikuwa limenifikia.


Basi, nikakuwa muchungaji wa kondoo ambao wachuuzi waliwatayarisha kwenda kuchinjwa. Nikatwaa fimbo mbili: moja nikaiita “Rehema”, na ingine nikaiita “Umoja”, nikaenda kuchunga kondoo.


Mukimbie huko na huko katika Yerusalema, mupeleleze na kujionea wenyewe, muchunguze katika masoko yake. Mukiona hata mutu mumoja anayefuata sheria, mutu anayetafuta ukweli, basi Yawe atausamehe Yerusalema.


Basi, wale vijana wa Daudi walirudi na kumwambia Daudi namna walivyojibiwa.


Nimepinduka mpaka chini na kupondekana; muchana kutwa ninazunguka nikiomboleza.


Na mwingine akamwambia: ‘Mimi ninatoka kuoa siku hizi, na kwa sababu hii siwezi kuja.’


Kisha, yule mutumishi akarudia na kusema: ‘Bwana, nimetimiza sawa ulivyoniamuru, lakini kungali nafasi.’


Nao wakamujibu: ‘Kwa sababu hakuna mutu aliyetupatia kazi.’ Halafu akawaambia: ‘Ninyi vilevile muende kutumika katika shamba langu la mizabibu.’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite