Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 14:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Mutu mumoja kati ya wale waliokuwa wakiikaa kula pamoja na Yesu aliposikia maneno hayo, akamwambia: “Heri mutu atakayeshiriki kwa kula karamu katika Ufalme wa Mungu!”

Gade chapit la Kopi




Luka 14:15
8 Referans Kwoze  

Halafu malaika akaniambia: “Andika maneno haya: Heri wale wanaoalikwa kwa karamu ya ndoa ya Mwana-Kondoo.” Naye akasema tena: “Maneno haya ni ya kweli yanayotoka kwa Mungu.”


kusudi mupate kula na kunywa pamoja nami katika ufalme wangu. Mutaikaa vilevile juu ya viti vya kifalme, kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.”


Watu watakuja toka mashariki na magaribi, kaskazini na kusini, nao wataikaa kula chakula katika Ufalme wa Mungu.


Wale wajinga walipokwenda kununua mafuta, bwana-arusi akafika. Wale wenzao watano waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika karamu ya ndoa. Kisha mulango ukafungwa.


Heri watumishi wale bwana wao atakaowakuta wakikesha wakati anapofika! Kweli ninawaambia: atafunga mukaba wake vizuri na kuwakaribisha kula chakula, na kubakia pale akiwashugulikia.


Ninawaambia wazi kwamba watu wengi watakuja toka mashariki na magaribi, nao watachangia meza pamoja na Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwenye karamu katika Ufalme wa mbinguni.


Kwa maana ninawaambia, sitakula tena karamu hii ya Pasaka mpaka siku ile nitakapokula ile yenye kukamilika katika Ufalme wa Mungu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite