Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 14:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”

Gade chapit la Kopi




Luka 14:11
24 Referans Kwoze  

Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Na yeyote anayejiinua, atashushwa, lakini anayejishusha, atainuliwa.


Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima.


Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Majivuno ya ndani ya moyo yanaleta maangamizi, lakini unyenyekevu unaleta heshima.


Mujinyenyekeze mbele ya Bwana, naye atawainua.


Ee Yawe, ingawa wewe uko juu ya wote, unawaangalia wanyenyekevu kwa wema; lakini, unatambua wenye kiburi kwa mbali.


Kiburi cha wanadamu kitashushwa, majivuno ya watu yatanyenyekezwa, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


bila kosa kwa wale ambao hawafanyi makosa, lakini mukali kwa waovu.


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Kumwogopa Yawe ni mafundisho ya hekima; mbele ya kuheshimika inafaa kuwa munyenyekevu.


Maana, Mungu anawashusha wenye majivuno, lakini anawaokoa wanyenyekevu.


Samweli akamwambia: “Ingawa unajiona kwamba wewe ni mudogo, lakini si wewe kiongozi wa makabila ya Israeli? Yawe alikupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme juu ya Israeli.


Ametenda kwa uwezo wake mukubwa, amewasambaza wale wanaofanya mipango kwa kiburi.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Wewe unawaokoa wanyenyekevu, lakini unaangalia wenye majivuno kusudi uwashushe.


Si vizuri kula asali nyingi sana; vilevile haifai kujipendekeza sana.


Amewashusha wafalme wenye uwezo, lakini amewainua wanyenyekevu.


Kisha Yesu akamwambia yule aliyemwalika: “Wakati unapofanya karamu ya muchana au ya magaribi, usiwaalike warafiki zako, wala wandugu zako, wala watu wa jamaa yako, wala jirani zako wanaokuwa watajiri, kusudi nao vilevile wasikualike, nawe usikuwe kama umelipwa.


Ndugu anayekuwa masikini afurahi kwa sababu Mungu anamupandisha,


Basi mujinyenyekeze mbele ya Mungu mwenye uwezo, kusudi awainue kwa wakati unaofaa.


Hapo mufalme akamwambia Hamani: “Fanya haraka! Twaa nguo hizi na farasi, umupatie Mordekayi heshima hii, yule Muyuda ambaye anaikaa kwenye mulango wa nyumba ya kifalme. Usiache kumufanyia hata jambo moja kati ya hayo uliyoyataja.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite