23 Mutu mumoja akamwuliza: “Bwana, ni watu wachache tu ndio watakaookolewa?” Halafu Yesu akawaambia:
Lakini njia inayoongoza kufikia kwenye uzima ni yenye kusongamana na mulango unaoiingilia ni mwembamba, nao watu wanaoifuata ni wachache tu.
Kisha, Yesu akasema: “Watu wanaoitwa ni wengi, lakini wale wanaochaguliwa ni wachache.”
Yesu akaongeza kusema: “Ni hivi inavyokuwa vilevile: wanaokuwa wa mwisho watakuwa wa kwanza, nao wanaokuwa wa kwanza watakuwa wa mwisho.”
Wanafunzi waliposikia maneno haya, wakashangaa sana na kuuliza: “Ni nani basi anayeweza kuokolewa?”
Yesu alipokuwa katika safari kwenda Yerusalema, alipita katika miji na vijiji akifundisha.
“Mufanye nguvu muingie kwa kupitia mulango unaokuwa mwembamba; maana ninawaambia ninyi hakika: watu wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.