Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 13:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Yesu aliposema vile, wapinzani wake wote wakafezeheka, lakini kundi lote la watu wote walifurahia matendo yote ya ajabu aliyoyatenda.

Gade chapit la Kopi




Luka 13:17
19 Referans Kwoze  

mukiwa na zamiri safi, hata wale wanaowasingizia na kuwatukana juu ya mwenendo wenu muzuri katika ushirika wenu na Kristo, wapate haya.


Waadui zake nitawavalisha haya; lakini yeye nitamuvalisha utukufu wa kifalme.”


Lakini hawataendelea mbali sana, kwa sababu upumbafu wao utaonekana wazi mbele ya watu wote, sawa ilivyokuwa kwa Yane na Yambure.


Kisha wale wakubwa wa baraza wakawakataza tena kwa ukali na kuwaachilia kwenda. Hawakupata njia ya kuwaazibu kwa maana watu wote walikuwa wakimusifu Mungu kwa ajili ya jambo lile lililotendeka.


Na hakuna mutu aliyesubutu tena kumwuliza maneno mengine.


Lakini hawakupata namna ya kumwua, kwa sababu watu wote walimusikiliza kwa uangalifu.


Na pale pale akapata kuona, na kumufuata Yesu akishukuru Mungu. Na watu wote walipoona jambo hili wakamusifu Mungu.


Nao hawakuweza kumujibu neno.


Watasema juu yangu: Haki na nguvu viko kwa Yawe peke yake. Wote waliomukasirikia Yawe watakuja kwake na haya.


Siku ile, tawi Yawe atakalochipuza litakuwa zuri na tukufu, nayo matunda ya inchi yatakuwa na heshima na utukufu kwa wale Waisraeli watakaobaki. Waisraeli watakaobaki watasifiwa na kujivunia mazao ya inchi yao.


Kila anachofanya kimejaa utukufu na heshima; haki yake inadumu milele.


Waadui zangu wazungukwe na mazarau; wajifunike haya yao kama vile nguo.


Upendezwe, ee Yawe, kuniokoa; ee Yawe, ukuje haraka kunisaidia.


“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?


Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!


Ufundishe maneno ya kweli watu wasiyoweza kubishia, hata wale wanaokupinga wapate haya kwa kukosewa na neno baya la kusema juu yetu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite