Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 13:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Lakini Bwana akamujibu: “Ninyi wanafiki! Kuna mutu mumoja kati yenu anayekosa kumufungua ngombe au punda wake toka katika upango kwa siku ya Sabato kwa kumupeleka kunywa maji?

Gade chapit la Kopi




Luka 13:15
16 Referans Kwoze  

Kisha akawaambia wale watu: “Ni nani kati yenu mutoto wake au ngombe wake akitumbukia ndani ya kisima, atakayekosa mara moja kumwondosha mule hata ikiwa ni siku ya Sabato?”


Ni vile ninyi munavyokuwa, kwa inje munaonekana kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini ndani yenu munajaa unafiki na uovu.


Wakati ule ule makundi mengi ya maelfu ya watu walikusanyika hata wakakanyaganakanyagana. Yesu akaanza kwanza kusema na wanafunzi wake, akiwaambia: “Mufanye angalisho na chachu ya Wafarisayo, maana yake unafiki wao.


Au, namna gani unaweza kumwambia ndugu yako kwamba aache umwondoe vumbi inayokuwa ndani ya jicho lake, wakati ndani ya jicho lako mungali ile nguzo. Wewe munafiki, ondosha kwanza nguzo kutoka ndani ya jicho lako, kisha utaweza kuona waziwazi na kuweza kuondosha ile vumbi inayokuwa ndani ya jicho la ndugu yako.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”


Ninyi wanafiki! Isaya alitabiri vema juu yenu, wakati aliposema maneno haya:


Wewe munafiki, ondosha kwanza nguzo kutoka ndani ya jicho lako, kisha utaweza kuona waziwazi na kuweza kuondoa ile vumbi inayokuwa ndani ya jicho la ndugu yako.


Watesaji watatoweka, wenye kumuchekelea Mungu watakwisha, wote wanaokusudia kutenda maovu watateketezwa.


Asiyemwogopa Mungu anaangamiza wengine kwa kinywa chake, lakini mwenye haki anaokolewa kwa maarifa yake.


Anafanya hivyo, mutu mubaya asitawale, au wale wanaohatarisha maisha ya watu.


Bwana alipomwona yule mama, akamusikilia huruma na kumwambia: “Usilie.”


na kuwatuma kwa Bwana kumwuliza: “Wewe ndiwe yule aliyepaswa kuja kutuokoa au tumungojee mwingine?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite