49 “Nimekuja kuleta moto katika dunia, nami ningetaka sana kuona ukiwa umekwisha kuwaka!
Atawaamulia wamasikini kwa haki na kutetea haki za wakosefu katika inchi. Kwa neno lake dunia itaazibiwa, kwa pumzi yake waovu watauawa.
Imetupasa kufanya kazi za yule aliyenituma wakati kungali muchana, kwa sababu usiku unakaribia, wakati mutu asipoweza kutumika.
Lakini kwa ngambo ingine, yule asiyejua mapenzi ya bwana yake, na anayefanya mambo yanayostahili azabu, atapigwa fimbo chache. Kwa maana kila mutu aliyepewa vingi, ataombwa kutoa vingi zaidi; na aliyepewa madaraka mengi, ataulizwa mengi zaidi.
Niko na muzigo wa mateso ninaopaswa kubeba, nami ninasongwa sana mpaka mapaswa hayo yatakapotimizwa!