Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 12:42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

42 Bwana akajibu: “Ni nani basi anayekuwa musimamizi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kwa kuwasimamia watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho lao kwa wakati uliopangwa.

Gade chapit la Kopi




Luka 12:42
29 Referans Kwoze  

Mutii waongozi wenu na kushika maagizo yao. Kwa maana wao wanashugulika kila mara kwa ajili ya roho zenu, na wao wanapaswa kutoa habari ya kazi yao mbele ya Mungu. Kwa kufanya vile mutawaruhusu kufanya kazi yao kwa furaha wala si kwa huzuni, kwa maana haitawafalia kitu kama wakitumika katika huzuni.


Muwakumbuke waongozi wenu waliowatangazia neno la Mungu. Muangalie vizuri namna walivyoishi na kufa. Mufuate imani yao.


utangaze Neno la Mungu kwa nguvu kwa wakati unaofaa na kwa wakati usiofaa. Ukaripe, usahihishe na kuonya ukifundisha kwa uvumilivu.


Wazee wa kanisa wanaoongoza kazi yao vizuri wanastahili kupokea mushahara mara mbili, hasa zaidi wale wanaojitolea kwa kufanya kazi ya kuhubiri na kufundisha.


Kila mutu kati yenu anapaswa kuitumia zawadi ya kiroho aliyojaliwa na Mungu kwa ajili ya mafaa ya wengine. Na hivi mutakuwa walinzi wazuri wa zawadi mbalimbali mulizopewa na Mungu.


Kwa maana musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno, kwa sababu yeye ni mwangalizi wa kazi ya Mungu. Hapaswi kuwa mutu mwenye kiburi, wala mukali, mulevi, mugomvi wala mwenye kutafuta mali kwa njia mbaya.


Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


“Ilipokuwa magaribi, mwenye shamba akamwambia musimamizi wake: ‘Uwaite watumishi na uwalipe mushahara wao, ukianzia kwa wale wa mwisho mpaka kwa wale wa kwanza.’


Munakunywa maziwa, munavaa nguo za manyoya yao na munawachinja kondoo wanono na kuwakula. Lakini hamuwakulishi hao kondoo.


Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Kutoa jibu zuri kunafurahisha; neno linalofaa kwa wakati wake ni jema sana!


Musa alikuwa mutumishi mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu, kusudi ashuhudie maneno ambayo Mungu angesema nyuma.


Lakini, kama nikikawia kufika, utaweza hivi kujua mwenendo unaopaswa kuwa nao katika nyumba ya Mungu, maana yake katika jamaa ya Mungu Mwenye Uzima. Yeye ndiye anayekuwa nguzo na musingi wa kweli.


Bwana alipomwona yule mama, akamusikilia huruma na kumwambia: “Usilie.”


Kisha akawaambia: “Basi, kila mwalimu wa Sheria aliyefundishwa katika Ufalme wa mbinguni, anafanana na mwenye nyumba anayetwaa vitu vipya na vitu vya zamani pamoja toka katika akiba yake.”


Nitawapa wachungaji watakaowatunza vema, nao hawatakuwa na woga tena wala kufazaika, na hakuna hata mumoja wao atakayepotea. –Ni ujumbe wa Yawe.


Anayetunza muti wa tini atakula matunda yake. Anayetumikia bwana wake ataheshimiwa.


Anaamuka mbele ya mapambazuko kwa kutayarishia jamaa yake chakula na kuwagawanyia kazi watumishi wake.


na kuwatuma kwa Bwana kumwuliza: “Wewe ndiwe yule aliyepaswa kuja kutuokoa au tumungojee mwingine?”


Heri mutumishi yule, ikiwa saa bwana wake anaporudia, anamukuta akifanya kazi ile.


Watu wote wenye ujuzi waliokuwa wanafanya kazi za kila namna za kujenga hema la mukutano walitoka, kila mumoja katika kazi yake, wakamwendea


Mutu anasifiwa kadiri ya hekima yake, lakini mwenye moyo wa mafikiri mabaya anazaruliwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite