Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 12:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Heri watumishi wale bwana wao atakaowakuta wakikesha wakati anapofika! Kweli ninawaambia: atafunga mukaba wake vizuri na kuwakaribisha kula chakula, na kubakia pale akiwashugulikia.

Gade chapit la Kopi




Luka 12:37
25 Referans Kwoze  

Kwa sababu hiyo, wapendwa wangu, mukiwa munangojea mambo yale, mufanye bidii apate kuwakuta safi bila kosa lolote na mukae na amani pamoja naye.


Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku Bwana wenu atakaporudi.


Maana ninasongwa na mambo mawili. Ninatamani kujiendea na kukaa pamoja na Kristo, maana hili ndilo jambo bora zaidi.


Lakini ni kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kuyaona wala kuyasikia, mambo yale ambayo hakuna mutu aliyepata kufikiri juu yake, ndiyo yale Mungu aliyowatayarishia wale wanaomupenda.”


Tena nikasikia sauti kutoka mbinguni, ikisema: “Andika maneno haya: ‘Heri tangu sasa kwa watu wanaokufa wakimwamini Bwana!’ ” Naye Roho anasema: “Ndiyo, ni kweli. Watapumzika toka katika masumbuko yao, kwa maana matendo yao yatafuatana nao.”


Maana kwa kufanya vile, mutaruhusiwa kabisa kuingia katika Ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Basi mukeshe na kuomba kila wakati, kusudi mupate nguvu ya kuepuka mambo hayo yote yatakayotokea, nanyi mupate kuweza kusimama mbele ya Mwana wa Mutu.”


Maana kama vile kijana mwanaume anavyomwoa binti, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi anavyofurahi juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.


Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


Hivi kwangu kuishi ni kwa ajili ya Kristo na kufa ni faida.


Si vile, yeye atamwambia kwanza amupigie chakula na kujitayarisha vizuri kusudi amushugulikie mpaka atakapomaliza kula na kunywa. Kisha pale, ataweza kula na kunywa.


Heri mutumishi yule, ikiwa saa bwana wake anaporudia, anamukuta akifanya kazi ile.


Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,


Nitafurahi kuwatendea mema; nitawasimika siku zote katika inchi hii na kuwatendea kwa uaminifu.


Mukuwe kama watumishi wanaomungojea bwana wao arudie kutoka katika karamu ya ndoa, kusudi wakati anapofika na kupiga hodi wamufungulie mulango mara moja.


Kwa maana, ni nani anayekuwa mukubwa; yule anayeikaa kwa kula chakula au yule anayemushugulikia? Hakika ni yule anayeikaa kwa kula chakula. Ingawa vile mimi niko hapa katikati yenu kama mwenye kushugulika!


“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite