Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Hakuna kitu chochote kinachofichwa kitakachokosa kuvumbulikana wala hakuna siri itakayokosa kujulikana.

Gade chapit la Kopi




Luka 12:2
10 Referans Kwoze  

Ni hivi vilevile hakuna chochote kinachofichwa kitakachokosa kuonekana wazi, wala hakuna siri itakayokosa kufunuliwa waziwazi.


Na ni hivi hakuna chochote kinachofichwa kitakachokosa kuonekana wazi, wala hakuna siri itakayokosa kufunuliwa waziwazi.


Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.


Maana, Mungu atahukumu matendo yote, hata yale yanayotendwa kwa siri, yakuwe mazuri au mabaya.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Hiyo ndiyo itakayotokea siku ile Mungu atakapohukumu mambo ya siri ya watu kwa njia ya Yesu Kristo, kama vile Habari Njema yangu inavyosema.


Maana, mimi ninayaona matendo yao yote, hakuna hata moja linalofichama mbele yangu. Maovu yao yote ni wazi mbele yangu.


Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite