Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 12:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Yeye akawaza na kusema: ‘Nitafanya nini hivi ninakosewa nafasi ya kuwekea mavuno yangu yote?’

Gade chapit la Kopi




Luka 12:17
23 Referans Kwoze  

Mutu akikuomba kitu, umupe. Na mutu akitaka umukopeshe, usimugeuzie mugongo.


Mafungo ya kweli ni kugawanya chakula chako pamoja na wenye njaa, kuwakaribisha katika nyumba yako wamasikini wasiokuwa na makao, kuwavalisha wasiokuwa na nguo, bila kusahau kuwasaidia wandugu zenu.


Sisi tumetambua upendo kwa njia hii: Yesu Kristo alitoa uzima wake kwa ajili yetu. Nasi vilevile tunapaswa kutoa uzima wetu kwa ajili ya wandugu zetu.


Muwasaidie watu wa Mungu katika mahitaji yao na muwakaribishe wageni.


Kisha akawapeleka inje na kuwauliza: “Wabwana wangu, inanipasa kufanya nini kusudi nipate kuokolewa!”


Naye akamwambia: ‘Ni vizuri wewe mutumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, ninakupa utawala juu ya miji kumi.’


Yesu aliposikia maneno haya, akamwambia: “Ungali unakosewa na kitu kimoja tu: uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudie unifuate!”


Yesu akaongeza kusema: “Nami ninawaambia: mutumie mali ya dunia hii kwa kuunga urafiki, kusudi wakati mali ile itakapokosekana, mupate kupokelewa kwenye makao ya milele.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Nao watu waliposikia maneno hayo, wakachomwa katika mioyo yao na kuwaambia Petro na mitume wengine: “Wandugu zetu, tufanye nini?”


Yule mulinzi akajiuliza: ‘Sasa nitafanya nini? Bwana wangu ananifukuza kwa kazi. Kulima, mimi siwezi; na kuombaomba, ninasikia haya.


Muuzishe vitu munavyokuwa navyo, muwasaidie wamasikini. Mujiwekee feza zisizoweza kuwa na upungufu, nayo akiba isiyoweza kumalizika katika mbingu. Kule wizi hawawezi kukaribia wala nondo hawaharibu.


Basi musijisumbue kwa kutafuta chakula au kinywaji.


Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ni kwa sababu hii ninawaambia: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwamba mutakula nini; wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu, kwamba mutavaa nini.


Basi muwasaidie wamasikini na vitu vya ndani, na vingine vyote vitakuwa safi kwenu.


Halafu mwalimu mumoja wa Sheria akasimama na kumwuliza Yesu kwa kumupima: “Mwalimu, nifanye nini kusudi nipate uzima wa milele?”


Naye akawajibu: “Mwenye kuwa na kanzu mbili atoe moja kwa yule asiyekuwa na kitu, na anayekuwa na vyakula afanye hivi vilevile.”


Gawa sehemu moja kwa watu saba hata wanane, maana, haujui hasara itakayofika katika dunia.


Wanafunzi wakaanza kusemezana hivi wao kwa wao: “Anasema hivi kwa sababu hatuna mikate.”


Halafu akawaambia mufano huu: “Kulikuwa tajiri mumoja aliyekuwa na shamba lenye kutoa mavuno mengi.


Kisha akajisemesha: ‘Nitafanya hivi: nitabomoa gala zangu na nitajenga zingine kubwa zaidi, na mule nitaweka mavuno yangu yote na mali zangu zingine.’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite