Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 11:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Nami ninawaambia: muombe nanyi mutapewa; mutafute nanyi mutapata; mupige hodi nanyi mutafunguliwa mulango.

Gade chapit la Kopi




Luka 11:9
40 Referans Kwoze  

Ni kwa hiyo ninawaambia kwamba munapoomba kwa ajili ya hitaji la kitu fulani, mwamini kama mumekwisha kukipokea, na kwa njia hiyo mutakipewa.


Na kitu chochote mutakachoomba, mukiamini, mutakipata.”


Ninyi hamukunichagua mimi, lakini ni mimi niliyewachagua ninyi. Nami nimewatuma muende kuzaa matunda yasiyokuwa na mwisho. Kwa hiyo Baba atawapa chochote munachoomba kwa jina langu.


Kama mukikaa ndani yangu na maneno yangu yanakaa ndani yenu, mutaomba chochote munachotaka, nanyi mutakipewa.


Nami nitafanya chochote mutakachoomba kwa jina langu, kusudi Baba atukuzwe kwa njia ya Mwana.


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.


Katika taabu yangu nilimwomba Yawe, naye akanisikia na kuniweka huru.


Kwa hiyo mutakapokuja kunililia na kuniomba, nitawasikiliza.


Basi pasipo imani, hakuna mutu anayeweza kumupendeza Mungu. Kwa maana mutu anayetaka kumwendea Mungu sherti aamini kwamba Mungu yuko, na kwamba anawapa zawadi wale wanaomutafuta.


Nao wakiomba kwa imani, mugonjwa yule atapona, kwa kuwa Bwana atamurudishia afya yake. Na ikiwa amefanya zambi, atasamehewa.


Uniite, nami nitakujibu na kukuambia mambo makubwa yaliyofichwa ambayo haujapata kuyajua.


Mumwabudu Yawe, enyi watakatifu wake, maana wenye kumwabudu hawakosewi kitu.


Kwa sababu hii, tujongelee kwa uhodari kiti cha kifalme cha Mungu pahali anapowajalia watu neema kusudi apate kutuhurumia na kutujalia neema ya kutusaidia kwa wakati unaofaa.


Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Mumutukuze Yawe pamoja nami, wote pamoja tulisifu jina lake.


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


Moyo wangu unaniambia: “Kuja umutafute Mungu!” Basi, ninakutafuta, ee Yawe.


Lakini ninawaambia kwamba hata mufalme Solomono katika utukufu wote aliokuwa nao hakuvaa nguo inayoweza kulinganishwa na uzuri wa moja la maua yale.


Kwa maana Mungu anasema hivi katika Maandiko Matakatifu: “Kwa wakati uliofaa, nilijibu maombi yako. Kwa siku ya wokovu, nilikusaidia.” Basi sasa, huu ndio wakati unaofaa, sasa leo ni siku ya wokovu.


Mambo ninayowaambia ninyi, ninayasema kwa wote: mukeshe.”


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Jambo moja nimemwomba Yawe, ninatafuta hili tu: nikae ndani ya nyumba ya Yawe siku zote za maisha yangu, niuone uzuri wa Yawe, na kutafuta maongozi yake ndani ya hekalu lake.


Nilimwomba Yawe, kwa moyo, nikimutolea maombi pamoja na kufunga kula chakula, nikavaa gunia na kuikaa kwenye majivu.


Kati ya hawa wawili ni nani aliyefanya sawa na mapenzi ya baba yake?” Wale wakubwa wakajibu: “Ni yule wa kwanza.” Na Yesu akawaambia: “Kweli ninawaambia: Walipishaji wa kodi pamoja na makahaba wataingia mbele yenu katika Ufalme wa Mungu.


Mimi sikusema kwa siri, wala katika inchi yenye giza. Mimi sikuwaambia wazao wa Yakobo wanitafute pahali kusipokuwa kitu. Mimi Yawe ninasema ukweli, maneno yangu ni ya kuaminika.


“Lakini ninyi watu wengine wa kanisa la Tuatera musiofuata hayo mafundisho ya Yezebeli, na ambao hamujui ile wanayoita ‘Siri za Shetani’, ninawaambia ninyi kama sitawabebesha muzigo mwingine.


Nikamufungulia mupenzi wangu mulango, lakini kumbe, alikuwa amekwisha kutoweka. Moyo wangu ulifurahi alipokuwa akizungumuza! Nikamutafuta, lakini sikumupata; nikamwita, lakini hakuniitikia.


Kwa maana kila mutu anayeomba anapewa; anayetafuta anapata, anayepiga hodi anafunguliwa mulango.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite