Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 11:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 Basi muwasaidie wamasikini na vitu vya ndani, na vingine vyote vitakuwa safi kwenu.

Gade chapit la Kopi




Luka 11:41
37 Referans Kwoze  

Muuzishe vitu munavyokuwa navyo, muwasaidie wamasikini. Mujiwekee feza zisizoweza kuwa na upungufu, nayo akiba isiyoweza kumalizika katika mbingu. Kule wizi hawawezi kukaribia wala nondo hawaharibu.


Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.


Kila kitu ni safi kwa watu wanaokuwa safi. Lakini hakuna chochote kinachokuwa safi kwa watu wachafu na wasiomwamini Mungu, kwa maana akili na zamiri zao zimekuwa chafu.


Tena, musisahau kutenda mema na kusaidiana, maana sadaka za namna hii zinamupendeza Mungu.


Lakini ile sauti ikamurudilia, ikisema: “Vitu vilivyotakaswa na Mungu, usivihesabu kuwa vichafu.”


Yesu akaongeza kusema: “Nami ninawaambia: mutumie mali ya dunia hii kwa kuunga urafiki, kusudi wakati mali ile itakapokosekana, mupate kupokelewa kwenye makao ya milele.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Anayemusaidia masikini anamukopesha Yawe; Yawe atamulipa kwa tendo lake jema.


Anayemutesa muzaifu anamutukana Muumba wake, lakini anayemwonea huruma mukosefu anamutukuza Mungu.


Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.


Lakini Zakayo akasimama mbele ya Bwana na kumwambia: “Bwana! Ninawapa masikini nusu ya mali zangu, na kama nimetwaa kitu cha mutu kwa kumudanganya, nitamurudishia mara ine sawa na kitu kile.”


Yesu aliposikia maneno haya, akamwambia: “Ungali unakosewa na kitu kimoja tu: uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudie unifuate!”


Mutu akikuomba kitu, umupe. Na mutu akitaka umukopeshe, usimugeuzie mugongo.


Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini. Haki yake inadumu milele. Ana nguvu na sifa.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.


Yule aliyekuwa akiiba, asiibe tena, lakini ajikaze kufanya kazi peke yake kwa usawa kusudi apate kuwasaidia wakosefu.


Wanafunzi wakakusudia kutuma musaada kwa wandugu waamini waliokaa katika jimbo la Yudea, kila mumoja kwa kadiri alivyoweza kutoa.


Kwa maana mutakuwa na wamasikini pamoja nanyi siku zote, lakini mimi sitakuwa pamoja nanyi siku zote.


“Nyuma ya kupitisha miaka mingi mbali na muji, nilirudi kule Yerusalema kuwaletea watu wa taifa langu musaada wa mali na kumutolea Mungu sadaka.


Kwa wema na uaminifu mutu anaondoa uovu. Kwa kumwogopa Yawe anaepuka ubaya.


Kitu kile hakiingii ndani ya moyo wake, lakini kinaingia tu ndani ya tumbo na kisha kinatoka na kwenda katika choo.” (Kwa kusema hivi Yesu alionyesha kwamba vyakula vyote vinaruhusiwa kukuliwa.)


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite