Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 11:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Ninyi wapumbafu! Si Mungu aliyeumba inje ya mutu ndiye aliyeumba ndani yake vilevile?

Gade chapit la Kopi




Luka 11:40
17 Referans Kwoze  

Lakini Mungu akamwambia: ‘Mupumbafu wewe! Leo leo usiku utakufa. Na sasa, vitu hivi vyote ulivyojitayarishia vitakuwa vya nani?’ ”


Wewe mujinga! Wakati unapopanda mbegu, mbegu ile haiwezi kuota isipokufa kwanza.


Wewe kipofu Mufarisayo! Safisha kwanza ndani ya kikombe na ya sahani, na kisha inje yake kutakuwa safi vilevile.


Na ikiwa wababa zetu wa kimwili walituadibisha, nasi tuliwaheshimu, jambo hilo halionyeshi zaidi kwamba tunapaswa kumuheshimu Baba yetu wa kiroho na kupata kuishi?


Basi Yesu akawaambia: “Enyi wajinga na wenye mioyo mizito kwa kuamini maneno yote manabii waliyosema!


Ninyi wapumbafu na vipofu! Ni nini inayokuwa kubwa zaidi, zahabu au hekalu linaloifanya zahabu ile ihesabiwe kuwa takatifu?


Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:


Musikilize, enyi wajinga na wapumbafu: ninyi munaokuwa na macho, lakini hamwoni, munaokuwa na masikio, lakini hamusikii.


Enyi wajinga, mujifunze kuwa na akili; musikilize kwa uangalifu, enyi wapumbafu.


“Enyi wajinga! Mpaka wakati gani mutapenda kuwa wajinga? Mpaka wakati gani wenye kuzarau watafurahia mazarau yao, na wapumbafu kuchukia maarifa?


Yeye anaunda mioyo ya watu wote, yeye anajua kila kitu wanachofanya.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Mupumbafu anajisemesha hivi katika moyo: “Hakuna Mungu.” Wote wamepotoka kabisa, matendo yao ni ya kuchukiza; hakuna hata mumoja anayetenda mazuri!


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Halafu Yawe Mungu akamwumba mwanaume kwa udongo, akamupulizia ndani ya pua pumzi ya uzima, na yule mwanaume akakuwa kiumbe chenye uzima.


Kisha Mungu akasema: “Tumufanye mutu kwa mufano wetu, anayefanana nasi, atawale samaki wa bahari, ndege wa anga, nyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vinavyotambaa.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite