Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 11:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako likiwa zima, mwili wako wote utabaki katika mwangaza. Lakini kama jicho lako linaharibika, mwili wako vilevile utabaki katika giza.

Gade chapit la Kopi




Luka 11:34
28 Referans Kwoze  

kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Uyafungue macho yangu, nipate kuona maajabu ya sheria yako.


Ninyi watumwa, muwatii wabwana wenu katika mambo yote hapa katika dunia. Musiwatii tu wakati wanapowaangalia ninyi kama mungetaka tu kujipendeza mbele yao, lakini muwatii kwa moyo mwema, kwa sababu munamuheshimu Bwana.


Lakini ninaogopa kwamba sawa vile nyoka alivyomudanganya Eva kwa werevu wake, mawazo yenu vilevile yasipotoshwe hata mupate kupoteza uaminifu na ukamilifu wenu kwa Kristo.


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Musikilize, enyi wajinga na wapumbafu: ninyi munaokuwa na macho, lakini hamwoni, munaokuwa na masikio, lakini hamusikii.


Ninamwomba Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye utukufu, awapatie Roho wake kusudi mukuwe na hekima na ufunuo hata muweze kumujua.


kusudi ‘Wapate kuangalia, lakini wasione; nao wapate kusikia, lakini wasikuwe na ufahamu, kusudi wasipate kumugeukia Mungu na kusamehewa.’ ”


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Muko na macho, lakini hamwoni? Muko na masikio, lakini hamusikii? Hamukumbuki


Watu hao hawajui wala hawaelewi kitu chochote. Wamefungwa macho wasipate kuona na akili wasipate kufahamu.


Basi, sasa Bwana atakuazibu, nawe utakuwa kipofu, wala hautaweza hata kidogo kuona mwangaza kwa muda.” Mara moja macho ya Elema yakaingiwa na giza hata yakapofuka, naye akaanza kupapasapapasa akitafuta mutu wa kumwongoza.


Yawe amewamwangia roho ya usingizi; macho yenu yasipate kuona enyi manabii, amefunika vichwa vyenu enyi wenye kupata maono.


Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona.


“Lakini watu wangu hawakunisikiliza; Israeli hakunitaka kabisa.


Ninyi watumwa, mutii wabwana wenu kwa woga na kutetemeka na kwa moyo wa ukweli kama vile munavyomutumikia Kristo.


Kila siku walikuwa wakikusanyika pamoja katika hekalu, nao walikula chakula pamoja katika nyumba zao kwa furaha na katika unyenyekevu.


uasherati, tamaa mbaya, matendo mabaya, ukorofi, maisha ya ovyo, wivu, matukano, majivuno na upumbafu.


Nani anayekuwa kipofu isipokuwa mutumishi wangu? Nani anayekuwa kiziwi kama mujumbe ninayemutuma? Ni nani anayekuwa kipofu kama huyu niliyemutakasa, au kipofu kama mutumishi wa Yawe?


Mutu muchoyo anakimbilia mali, wala hajui kwamba ukosefu utamufikia.


Kisha wakawapiga kwa kuwapofusha macho wanaume wote waliokuwa kwa mulango, wakubwa na wadogo, hata wakataabika kwa kutafuta ule mulango, nao hawakuupata.


Macho ya kiburi na moyo wa majivuno vinaonyesha wazi zambi ya waovu.


Ole kwao wanaosema ubaya ni uzuri na uzuri ni ubaya. Wanasema giza ni mwangaza na mwangaza ni giza. Wanasema kichungu ni kitamu na kitamu ni kichungu.


Ujiangalie vizuri kusudi mwangaza unaokuwa ndani yako usigeuke kuwa giza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite