Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 11:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Kwa Siku ya hukumu, watu wa Ninawe watasimama nanyi watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu wao waligeuka toka zambi zao waliposikia mahubiri ya Yona! Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kupita Yona!

Gade chapit la Kopi




Luka 11:32
9 Referans Kwoze  

Basi Yesu ndiye Kuhani Mukubwa anayefaa kwa ajili yetu. Yeye ni mutakatifu, hana kosa wala alama ya uchafu. Ametengwa mbali na wenye zambi, naye amenyanyuliwa juu sana mbinguni.


Vilevile kwa Siku ya hukumu, Malkia toka Kusini atasimama na watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu yeye alitoka mbali sana kuja kusikiliza maneno ya hekima ya mufalme Solomono. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kupita Solomono!


Lakini Mungu akamwuliza Yona: Unazani unafanya vema kuukasirikia mumea huo? Yona akajibu: Ndiyo, ninafanya vema kukasirika – kukasirika hata kufa!


Basi, watu wa Ninawe wakauamini ujumbe wa Mungu, wakatangaza kufunga kula chakula, na kwamba kila mumoja wao, mukubwa kama vile mudogo, avae gunia.


Alipofika, Yona aliingia katika muji. Kisha kutembea mwendo wa siku nzima, akaanza kutangaza: Kunabaki siku makumi ine tu na muji huu wa Ninawe utaangamizwa!


Yesu akawajibu: “Watu wa kizazi kibaya na kinachokosa uaminifu mbele ya Mungu, wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataona kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha nabii Yona.


Kwa Siku ya hukumu, watu wa Ninawe watasimama nanyi watu wa kizazi hiki na kuwashitaki, kwa sababu wao waligeuka toka zambi zao waliposikia mahubiri ya Yona. Hapa kuna yule anayekuwa mukubwa kupita Yona!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite