16 Na wengine walitaka kumupima wakimwomba awaonyeshe kitambulisho kinachohakikisha kwamba uwezo wake umetoka kwa Mungu.
Wakamwuliza: “Basi utatuonyesha kitambulisho gani kusudi tupate kukiona na kukuamini? Utafanya jambo gani?
Wayuda wanaomba kuonyeshwa vitambulisho nao Wagriki wanatafuta hekima.
Wakati watu wengi walipokuwa wakikusanyika pembeni ya Yesu, yeye akaanza kusema: “Watu wa kizazi hiki kibaya wanataka kuona kitambulisho. Lakini hawataonyeshwa kitambulisho isipokuwa kitambulisho cha Yona.
Wao walisema hivi kwa kumupima, kusudi wapate sababu ya kumushitaki. Lakini Yesu akainama na kuandika juu ya udongo kwa kidole chake.