Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 11:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, inaonyesha hakika kwamba Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa Roho Mutakatifu wale wanaomwomba kwake.”

Gade chapit la Kopi




Luka 11:13
30 Referans Kwoze  

Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, zaidi sana Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa wale wanaomwomba vitu vizuri zaidi.


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Musikilize maonyo yangu; nitawamiminia mawazo yangu, nitawajulisha maneno yangu.


Petro akawajibu: “Mugeuke toka katika zambi zenu, na kila mumoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo, na Mungu atawasamehe zambi zenu. Hivi mutapokea zawadi ya Roho Mutakatifu.


Nitatia roho yangu ndani yenu; nitawafanya mufuate masharti yangu na kushika maagizo yangu.


Lakini Yawe anasema: Munafikiri kwamba mama anaweza kumusahau mutoto anayemunyonyesha, wala kumuchukia mutoto wa tumbo lake? Hata kama mama anaweza kumusahau mutoto wake, mimi sitakusahau hata kidogo.


“Hivi, mukiwasamehe watu wengine makosa wanayowatendea, Baba yenu anayekuwa mbinguni atawasamehe vilevile.


Ni wapagani ndio wanaoshugulika kwa kutafuta vitu vile vyote. Baba yenu anayekuwa mbinguni anajua kama munahitaji vitu vile vyote.


Yesu akawaambia: “Munapoomba, museme: ‘Baba! Jina lako litukuzwe; Ufalme wako ukuje.


Basi ikiwa Mungu anavalisha majani kama hivi, yanayoonekana leo na kesho yanatoweka na kutupwa katika moto, hatawavalisha ninyi vizuri zaidi, ninyi wenye imani ndogo?


Mufanye vile kusudi mupate kuwa kweli watoto wa Baba yenu anayekuwa mbinguni. Kwa maana yeye anawaangazia waovu na wema jua lake, naye anawanyeshea mvua wenye haki na wasiokuwa wenye haki.


Vilevile, mwangaza wenu unapaswa kuangaza mbele ya watu, kusudi waone matendo yenu mazuri, nao wamutukuze Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Ninaitikia kabisa makosa yangu, siku zote ninaona waziwazi zambi yangu.


Kwa maana ninajua kwamba hakuna kitu kizuri kinachokaa ndani yangu, ni kusema katika hali yangu ya kimwili. Ni hivi kwa sababu ninakuwa na utashi wa kufanya jambo jema, lakini sifikii kulifanya.


Ni kweli kwamba kifo kilitawala kwa njia ya mutu mumoja, kwa sababu ya kosa la huyo mumoja. Lakini inaonyesha zaidi sana kwamba wale wanaopewa neema ya Mungu kwa uwingi na zawadi ya haki yake, wataishi na kutawala kwa njia ya mutu mumoja, Yesu Kristo.


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Au anayeweza kumupa nge kama akimwomba yai?


Basi, Mungu hatawapatia haki wale wachaguliwa wake wanaomulilia usiku na muchana? Au atakawia kuwasaidia?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite