Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 10:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Akajongea karibu naye, akamutunza vidonda, akivimwangia divai na kuvimimia mafuta na kuvifunga na vitambaa. Kisha akamupandisha juu ya punda wake, na kumupeleka kwenye nyumba ya kupangisha wageni na kumuchunga.

Gade chapit la Kopi




Luka 10:34
14 Referans Kwoze  

Lakini kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Adui yako akisikia njaa, umupe chakula; kama akisikia kiu, umupe kinywaji. Maana kwa kufanya hivi utamupatisha haya kama vile ungemubebesha makaa ya moto juu ya kichwa.”


Anawaponyesha waliovunjika moyo; na kuwatunza vidonda vyao.


Muangalie vema, hata mumoja wenu asimurudishie mwenzake ubaya kwa ubaya, lakini mutafutiane wema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.


Akazaa mwana, ndiye muzaliwa wake wa kwanza. Akamufunika nguo za kitoto na kumulalisha katika sanduku ya kukulishia nyama, kwa sababu walikosa nafasi ya kukaa katika nyumba ya kupangisha wageni.


Amefanya sawa alivyoweza. Ameupakaa mwili wangu marasi mbele ya wakati kwa kuutayarisha kwa ajili ya maziko.


Akiwa bado katika njia kurudi Misri, Musa alikuwa pahali pa kulala pa wageni. Basi, Mungu akakutana naye na kutaka kumwua.


Ikakuwa walipofika pahali pa kulala wageni kwa njia, mumoja wao akafungua mufuko wake kusudi apate kumukulisha punda wake, akashangaa kukuta feza yake kwenye kinywa cha mufuko wake.


Lakini Musamaria mumoja, alikuwa akisafiri vilevile katika njia ile, akafika kwenye nafasi ile yule mutu alipokuwa. Wakati alipomwona, akamusikilia huruma.


Kesho yake akatwaa vikoroti viwili vya feza, na kuvitoa kwa mwenye nyumba, akimwambia: ‘Umuchunge mutu huyu, na feza zingine utakazotumia zaidi ya hizi kwa matunzo yake, nitazilipa kwako nitakaporudia.’ ”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite