Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 10:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 Kukatokea kuhani mumoja akishuka katika njia ile ile. Wakati alipomwona yule mutu, akapita pembeni na kujiendea.

Gade chapit la Kopi




Luka 10:31
18 Referans Kwoze  

Wewe unajua ninavyotukanwa, unajua haya na matusi ninazopata; na waadui zangu wote wewe unawajua.


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Kama vile wanyanganyi wanavyomuvizia mutu katika njia, ndivyo makuhani walivyojikusanya na kuvizia. Wanaua watu katika njia yenye kuelekea Sekemu, na kutenda uovu mukubwa.


Musikilize, enyi makuhani! Mutege sikio, enyi Waisraeli! Musikilize, enyi ukoo wa kifalme! Ninyi mulipaswa kulinda haki, pahali pake mumekuwa kama mutego kule Misipa, mumekuwa kama wavu wa kuwanasa kule Tabori.


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja.


Anayekataa kusikia kilio cha masikini hatasikilizwa atakapolilia musaada.


Roho yangu inaporegea kabisa, yeye yuko, anajua mwenendo wangu. Waadui wamenitegea mitego katika njia ninayopita.


Basi Ruta akaenda katika shamba, akawafuata wavunaji naye akiyaokota masuke waliyoyaacha. Na kumbe akajikuta katika shamba la Boazi, yule wa ukoo wa Elimeleki.


Yule kijana akamujibu: “Kwa bahati, nilikuwa juu ya mulima Gilboa. Nilimwona Saulo akiegemea mukuki wake na magari ya waaskari wapanda-farasi ya waadui zake yalikuwa yanamusonga sana.


Mafungo ya kweli ni kugawanya chakula chako pamoja na wenye njaa, kuwakaribisha katika nyumba yako wamasikini wasiokuwa na makao, kuwavalisha wasiokuwa na nguo, bila kusahau kuwasaidia wandugu zenu.


Yesu akajibu akimwelezea: “Mutu mumoja alitoka Yerusalema akishuka kwenda Yeriko. Alipokuwa katika njia, akashambuliwa na wanyanganyi, wakamuvua nguo, wakamupigapiga, wakajiendea, wakimwacha karibu kufa.


Vilevile Mulawi mumoja akafika kwenye nafasi ile, naye alipomwona mutu yule, akapita pembeni na kujiendea.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite