Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 10:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Saa ile ile, Yesu akajazwa na furaha kwa uwezo wa Roho Mutakatifu, naye akasema: “Ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo. Ndiyo Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.

Gade chapit la Kopi




Luka 10:21
29 Referans Kwoze  

Lakini kama Habari Njema tunayotangaza ni ngumu kwa kusikia, ni kwa wale tu wanaofuata njia ya upotevu.


Mungu amefanya kila kitu kufuatana na kusudi na mapenzi yake. Yeye ametuchagua kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watu wake.


Mungu amekusudia tangu zamani kutukubali sisi kuwa watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Alifanya vile kufuatana na mapenzi yake.


Kweli ninawaambia ninyi: mutu yeyote asiyepokea Ufalme wa Mungu kama mutoto mudogo, hawezi kuingia ndani yake hata kidogo.”


Basi wakamwuliza Yesu: “Unasikia maneno watoto hawa wanayoyasema?” Yesu akawajibu: “Ndiyo. Lakini hamujasoma Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Kwa vinywa vya watoto wadogo hata wale wanaokuwa wachanga umetangaza sifa zako.’ ”


Halafu Yesu akamwambia: “Heri kwako, wewe Simoni mwana wa Yona, kwa maana hakuna mutu aliyekufunulia neno hili isipokuwa Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Ee Yawe, Bwana wetu, jina lako linatukuzwa sana katika dunia yote! Utukufu wako unaenea mpaka juu ya mbingu!


Anapokipata atawaita warafiki na jirani zake na kuwaambia: ‘Mufurahi pamoja nami kwa sababu nimepata kikoroti kile cha feza nilichokipoteza!’


Atakapomwona, atamubeba kwa furaha juu ya mabega.


Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,


Yawe anasema hivi: Mbingu ni kiti changu cha kifalme, dunia ni kiti cha kupumzikishia miguu yangu. Mutanijengea nyumba ya namna gani basi, pahali nitakapoweza kupumzikia?


Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.


Hivyo, nitawatendea tena watu hawa maajabu, mambo ya ajabu na ya kushangaza. Nao wenye hekima wao wataishiwa hekima, na akili ya wenye akili wao itatoweka.


Basi wakaondosha lile jiwe. Yesu akainua macho juu, akasema: “Baba, ninakushukuru kwa sababu umenisikia.


Maana kama vile kijana mwanaume anavyomwoa binti, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi anavyofurahi juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.


Humo kutakuwa barabara kubwa, nayo itaitwa Njia Takatifu. Watu wachafu hawatapitia humo, lakini wale watu wa Mungu tu; wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,


Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Zaburi ya Daudi. Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe; ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake.


Yoane alipoona Wafarisayo wengi na Wasadukayo wakimufikia kwa kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliyewaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite