Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Siku moja, Zakaria alikuwa akimutumikia Mungu, akifanya kazi yake ya ukuhani kwa maana ilikuwa zamu ya kundi lake.

Gade chapit la Kopi




Luka 1:8
16 Referans Kwoze  

Akifuata maagizo ya Daudi baba yake, alipanga zamu za kila siku za makuhani na za Walawi waliowasaidia makuhani kusifu na kutimiza kazi zao. Vilevile aliwapanga walinzi wa milango katika makundi aliyoweka kwa kulinda kila mulango; maana ndivyo Daudi, mutu wa Mungu alivyoamuru.


Hawa waliandikishwa kulingana na kazi zao kuingia katika nyumba ya Yawe kutumika kwa kadiri ya utaratibu waliowekewa na babu yao Haruni, kama vile alivyoamuriwa na Yawe, Mungu wa Israeli.


Mufalme Hezekia akawapanga tena makuhani na Walawi katika makundi, akamupa kila mumoja wao kazi kufuatana na utumishi wake katika sehemu mbalimbali za hekalu la Yawe. Kazi ile ni pamoja na utoaji wa sadaka za kuteketeza kwa moto na za amani, za shukrani na za kusifu.


Katika siku Herode alipokuwa mufalme wa Yudea, kulikuwa kuhani mumoja, aliyeitwa Zakaria, wa kundi la makuhani wa ukoo wa Abiya. Muke wake Elizabeti alikuwa vilevile wa uzao wa Kuhani Mukubwa Haruni.


Vilevile, kwa ajili ya kazi ya Mungu katika Yerusalema, waliwapanga makuhani katika makundi yao ya Walawi katika zamu zao kufuatana na maagizo yaliyoandikiwa katika kitabu cha Musa.


Vilevile, kati ya wazao wa Haruni, makuhani waliokuwa wanakaa katika mashamba waliyorizi kwa pamoja inje ya miji yao, kulikuwa watu waliochaguliwa kwenye miji hiyo ambao waliwagawanyia sehemu zao za vyakula. Waliwapa sehemu kila mwanaume katika jamaa za makuhani, na kila mumoja aliyekuwa ameandikishwa kati ya Walawi.


Walawi wakaacha mashamba yao ya malisho ya nyama, na maeneo yao mengine kwa sababu Yeroboamu na wana wake waliwakataza kumutumikia Yawe kama vile makuhani wa Yawe.


Lakini wewe peke yako na wana wako mutafanya kazi zote za kikuhani kwa ajili ya mazabahu na vyote vinavyokuwa ndani ya pazia. Hayo ni mapaswa yenu, kwa sababu ninawapa zawadi ya ukuhani. Mutu yeyote asiyestahili atakayekaribia vyombo vya hema, atauawa.


Kisha umupakae Haruni mafuta na wana wake na kuwatakasa kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


Hema la mukutano na mazabahu nitavifanya vitakatifu. Vilevile Haruni na wana wake nitawatakasa kusudi wanitumikie kama makuhani.


Utawafunga mikaba katika viuno na kuwavalisha kofia zao. Hivi ndivyo utakavyowatakasa Haruni na wana wake kuwa makuhani. Hao watakuwa makuhani siku zote kwa ajili ya sharti la siku zote.


Haya ndiyo mambo utakayowafanyia Haruni na wana wake kwa kuwatakasa wapate kunitumikia kama vile makuhani. Utatwaa mwana-ngombe dume na kondoo dume wawili wasiokuwa na kilema,


Utamuvalisha ndugu yako Haruni na wana wake nguo zile, kisha uwapakae mafuta na kuwawekea mikono kwa kuwatakasa wanitumikie kama vile makuhani.


Nawe Musa umulete kwangu Haruni ndugu yako, pamoja na wana wake: Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari. Utawachagua kati ya Waisraeli, kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


Nadabu na Abihu walikufa mbele ya baba yao, wala hawakukuwa na watoto; kwa hiyo wandugu zao Eleazari na Itamari wakakuwa makuhani.


Lakini hawakukuwa na mutoto, kwa maana Elizabeti alikuwa tasa, tena wote wawili walikuwa wazee sana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite