Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 1:79 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

79 Atawaangazia wale wanaoishi katika giza na wanaokaa katika kivuli cha kifo, kusudi atuongoze tupate kufuata njia ya amani.”

Gade chapit la Kopi




Luka 1:79
36 Referans Kwoze  

Wewe, ee Mungu, umeongoza taifa, umezidisha furaha yake. Watu wanafurahi mbele yako wana furaha kama kwa wakati wa mavuno, kama vile wanaogawanya vitu walivyonyanganya wanavyofurahi.


Watu hao wanaokaa katika giza, mwangaza umewatokea! Hao wanaoishi katika inchi yenye giza nzito sana ya lufu, wameona mwangaza mukubwa.”


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Zamani muliishi katika giza, lakini sasa, kwa kuungana kwenu na Bwana, munaishi katika mwangaza. Muishi kama watoto wa mwangaza,


Utayafungua macho ya vipofu, utawafungua wafungwa toka katika kifungo, utawaweka huru wale waliofungwa katika giza.


Mimi nimekuja katika dunia kama mwangaza, kusudi mutu yeyote anayeniamini asikae katika giza.


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Wakati nikingali katika dunia, mimi ni mwangaza wa dunia.”


Aliwatoa katika giza na ukiwa, na minyororo yao akaivunjavunja.


Wengine waliishi katika giza na ukiwa, wafungwa katika mateso na minyororo,


Utawaambia wafungwa: Mutoke humo katika kifungo na wale wanaokuwa katika giza: Mukuje inje kwenye mwangaza! Kila pahali watakapokwenda watapata chakula hata kwenye vilima vitupu watapata malisho.


Ule mwangaza wa kweli, unaomwangazia kila mutu, unakuja katika dunia.


Hata nikipita katika bonde la giza kubwa, sitaogopa hatari yoyote, maana wewe, ee Yawe, ni pamoja nami; gongo lako na fimbo yako vinanipa moyo.


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe aliyetuondoa katika inchi ya Misri, aliyetuongoza katika mbuga, katika inchi ya jangwa na mashimo, inchi inayokauka na yenye giza kubwa, inchi isiyopitiwa na mutu yeyote, wala kukaliwa na mwanadamu?


Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.


Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu, nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui. Mbele yao nitaligeuza giza kuwa mwangaza, na pahali penye kuharibika patakuwa laini. Huo ndio mupango wangu wa kufanya, nami nitautimiza.


hawawazi juu ya njia ya kuleta amani,


Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.


Njia ya amani hamuijui hata kidogo; hamufuati sheria ya Mungu. Mumejifanyia njia potovu, yeyote anayepitia humo hapati amani.


Lakini Yawe anasema hivi: Hakuna amani kwa watu waovu.


Hatujakuasi wewe, wala hatujaiacha njia yako.


Kila mutu anayemwabudu Yawe, Yawe atamufundisha njia ya kufuata.


Njia zake ni za kupendeza, zote zinaelekea kwenye amani.


inchi ya huzuni na fujo, ambako mwangaza wake ni kama giza.


Yawe, Mutakatifu wa Israeli, Mukombozi wako, anasema hivi: Mimi ndiye Yawe, Mungu wako; ninayekufundisha kwa faida yako na kukuongoza katika njia unayotakiwa kwenda.


Ninatembea katika njia ya haki; ninafuata sheria ya Mungu.


Itawaliwe na giza kubwa sana, mawingu mazito yaifunike. Giza la muchana liitishe!


Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite