Maneno yale yatatimia kwa wakati wake uliopangwa, lakini kwa sababu haukuyasadiki, utakuwa bubu. Hautaweza kusema mpaka siku ile mambo hayo yatakapotimia.”
Wakati Yesu alipokwisha kumufukuza yule pepo, yule bubu akaanza kusema. Nao watu wote wakashangaa na kusema: “Hatujaona jambo kama hili katika inchi yote ya Israeli!”
Lakini wakati nitakaposema nawe nitakifungua kinywa chako, nawe utawaambia kwamba: “Yawe anasema hivi”. Atakayesikia, asikie; atakayekataa kusikia, akatae; maana hao ni watu waasi.