Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 1:59 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

59 Ilipotimia siku nane tangu mutoto alipozaliwa, wakaenda kumutahiri, nao wakataka kumupa jina la baba yake Zakaria.

Gade chapit la Kopi




Luka 1:59
6 Referans Kwoze  

Mutoto huyo atatahiriwa katika siku yake ya nane.


Kila mutoto mwanaume kati yenu anapaswa kutahiriwa kwa umri wa siku nane. Vilevile watumwa waliozaliwa katika nyumba yenu au walionunuliwa kwa feza zenu kutoka kwa wageni wasiokuwa wa uzao wenu. Hiki ni kitambulisho cha agano langu katika miili yenu, agano la milele.


Nilitahiriwa nilipokuwa na umri wa siku nane. Mimi ni Mwisraeli, wa kabila la Benjamina, Mwebrania wa asili kabisa. Kuelekea mambo ya Sheria ya Kiyuda, nilikuwa Mufarisayo,


Ilipotimia siku ya kumutahiri mutoto, ndiyo siku ya nane tangu alipozaliwa, wakamupa jina lake Yesu. Jina hili ni lile malaika alilojulisha mbele mama yake hajabeba mimba.


Halafu Mungu akafanya agano na Abrahamu, na kitambulisho cha kuhakikisha kwamba limeshikwa kilikuwa kutahiriwa. Kwa hiyo Abrahamu akamutahiri mwana wake Isaka alipotimiza siku nane za kuzaliwa. Naye Isaka akamutahiri mwana wake Yakobo, na Yakobo akawatahiri wana wake kumi na wawili waliokuwa babu zetu wakubwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite