Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 1:58 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

58 Wajirani zake na wandugu zake wa jamaa waliposikia jinsi Bwana amemusikilia huruma sana, wakafurahi wote pamoja naye.

Gade chapit la Kopi




Luka 1:58
12 Referans Kwoze  

Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


“Sasa Bwana amenifanyia mema kwa kunitendea hivi; ameniondolea haya ya kutokuzaa niliyokuwa nayo mbele ya watu.”


Utakuwa na furaha na shangwe kwa ajili yake, na watu wengi watafurahia kuzaliwa kwake,


Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho.


Anamurudishia heshima mwanamuke anayekuwa tasa; anamufurahisha kwa kumujalia watoto. Haleluia!


Naye Sara akasema: “Mungu amenipatia kicheko; yeyote atakayesikia habari hizi, atacheka pamoja nami.”


Ni kweli kwamba mimi mutumishi wako nimepata kukubaliwa mbele yako, nawe umenitendea mema sana kwa kuokoa maisha yangu. Lakini kwenye milima ni mbali sana. Maangamizi haya yatanikuta mbele sijafika kule, nami nitakufa.


Wakati wa kuzaa kwa Elizabeti ulipotimia, akazaa mutoto mwanaume.


Kisha Yesu akamwambia yule aliyemwalika: “Wakati unapofanya karamu ya muchana au ya magaribi, usiwaalike warafiki zako, wala wandugu zako, wala watu wa jamaa yako, wala jirani zako wanaokuwa watajiri, kusudi nao vilevile wasikualike, nawe usikuwe kama umelipwa.


Uwafurahishe baba na mama yako; mama yako aliyekuzaa afurahi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite