Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 1:51 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

51 Ametenda kwa uwezo wake mukubwa, amewasambaza wale wanaofanya mipango kwa kiburi.

Gade chapit la Kopi




Luka 1:51
32 Referans Kwoze  

Zaburi. Mumwimbie Yawe wimbo mupya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu! Nguvu yake kubwa, mukono wake mutakatifu umemupatia ushindi.


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?


Ijapokuwa wanamujua Mungu, hawamutukuzi wala kumushukuru kama vile anavyostahili. Lakini mawazo yao yaligeukia mambo ya ovyo ovyo, na mioyo yao isiyokuwa na ufahamu ilibaki katika giza.


ambaye kwa mukono wake wenye nguvu alifanya maajabu kwa njia ya Musa, akapasua bahari na kuwaongoza watu wake, na kujipatia jina la milele?


Bwana wetu Yawe anakuja na nguvu, kwa mukono wake anatawala. Yeye anakuja na mapato yake, anafika na mushahara wake.


Sauti za furaha ya ushindi zikasikilika katika hema za watu wa haki: “Mukono wa Yawe umetenda mambo makubwa!


Wewe unaamuru machafuko ya bahari; mawimbi yake yakiinuka, unayatuliza.


Yawe alipoona uwingi wa uovu wa watu katika dunia, na kwamba kila kitu mwanadamu anachokusudia ndani ya moyo wake ni kiovu siku zote,


Kwa sababu hiyo, kwa muda wa siku moja tu utapatwa na mapigo ya mauti, huzuni na njaa. Na zaidi ya hiyo utateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana wetu, Mungu anayeuhukumu, ni mwenye uwezo.”


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


kuangusha vizuizo vyote watu wanavyojivunia kwa kupinga elimu ya Mungu. Tunatawala mafikiri ya watu na kuyafanya yapate kumutii Kristo.


Wewe uliumba kaskazini na kusini; milima Tabori na Hermoni inakushangilia.


Nitakushukuru maisha yangu yote, nitakuomba nikikuinulia mikono yangu.


“Muangalie yaliyomupata mutu huyu! Yeye hakutaka Mungu akuwe kimbilio lake, lakini alitegemea wingi wa mali yake, na kutafuta humo usalama wake!”


Yawe anavunja mipango ya mataifa, na anabadilisha mawazo yao.


Kuna Mungu yeyote mwingine aliyejaribu hata kidogo kwenda kujitwalia taifa lake kutoka taifa lingine, kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyofanya, kwa kutumia majaribio, vitambulisho, maajabu, vita, na vitisho? Hapana. Lakini mulishuhudia kwa macho yenu namna Yawe alivyofanya kwa mukono wake wenye nguvu kabisa kule Misri.


Sasa ninajua kwamba Yawe ni mukubwa kuliko miungu yote, maana amewakomboa watu hawa toka katika mikono ya Wamisri ambao waliwatendea ubaya.”


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Hivyo, Yawe akawatawanya pahali pote katika dunia, nao wakaacha kujenga ule muji.


Mimi Yawe nitakufanya wewe Edomu kuwa mudogo kuliko mataifa yote. Ulimwengu wote utakuzarau.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite