Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Luka 1:49 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

49 sababu Mungu Mwenye Uwezo, amenitendea maajabu. Jina lake ni takatifu.

Gade chapit la Kopi




Luka 1:49
21 Referans Kwoze  

Aliwakomboa watu wake na kufanya nao agano la milele. Yeye ni mutakatifu na wa kutisha sana!


Wote wasifu jina lake kubwa la kutisha. Yeye ni mutakatifu!


Ee Yawe, hakuna anayekuwa kama wewe; wewe ni mukubwa na nguvu yako inajulikana.


Basi, Mungu ambaye kwa nguvu yake inayofanya kazi ndani yetu, anaweza kufanya mambo makubwa zaidi yanayopita yale tunayoweza kuomba au kufikiri;


Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Ewe Bwana, hakuna asiyekuogopa, wala hakuna asiyekutukuza, kwa maana wewe peke yako ndiwe mutakatifu. Mataifa yote yatakuja kukuabudu, kwa maana matendo yako ya haki yameonyeshwa wazi.”


Mumusifu Yawe, Mungu wetu; muiname kwa mulima wake mutakatifu! Yawe, Mungu wetu, ni mutakatifu.


Hakuna anayekuwa mutakatifu kama Yawe; hakuna yeyote anayekuwa kama yeye; hakuna anayekuwa jiwe la kufichamia kama Mungu wetu.


“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?


Walilalamikiana mumoja kwa mwengine hivi: Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Yawe wa majeshi! Dunia yote imejaa utukufu wake.


Lakini wewe Yawe uko pamoja nami. Kwangu wewe ni kama shujaa wa kutisha. Kwa hiyo watesaji wangu watajikwaa, nao hawataweza kunishinda. Watafezeheka kabisa, kwa sababu hawatashinda. Haya yao itadumu hata milele, nayo haitasahauliwa.


Na kila kimoja cha viumbe vya ajabu kilikuwa na mabawa sita yenye kujaa macho ndani na inje. Navyo viliimba muchana na usiku bila kuchoka, vikisema: “Mutakatifu, mutakatifu, mutakatifu ni Bwana wetu, Mungu Mwenye Uwezo, aliyekuwa, anayekuwa na anayekuja.”


Yesu akawaruhusu. Halafu wale pepo wakatoka ndani ya mutu yule na kuingia ndani ya nguruwe. Kundi zima la nguruwe, karibu elfu mbili, wakatelemuka mbio kwenye mulima na kutumbukia ndani ya ziwa, nao wakazama ndani ya maji.


Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–


Ni nani huyo Mufalme mwenye utukufu? Ni Yawe, mwenye nguvu na uwezo; Yawe, mwenye uwezo katika vita.


Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, anayefika kutoka Bosira na nguo ya madoa mekundu? Ni nani huyo aliyevaa nguo ya utukufu, anatembea kwa nguvu zake kubwa? Ni mimi Yawe ninayetangaza ushindi wangu; nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.


kwa maana ameniangalia kwa huruma, mimi mujakazi wake munyenyekevu. Tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri,


Yeye anawasikilia wale wanaomwogopa huruma kwa vizazi vyote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite